BREAKING

Tuesday 25 August 2015

HUYU NDIYE JOHN POMBE MAGUFULI AFUNIKA KATAVI, SUMBAWANGA, AWA MALAIKA ATANGAZA VITA NA VIONGOZI WABADHIRIFU













MAMA SAMIA AITEKA MOSHI MJINI

 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu akihutubia maelfu ya wananchi kwenye mkutano wake wa kampeni aliofanya kwenye Viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi mjini mkoani Kilimanjaro, leo.
 Wananachi wakimpongeza mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo jimbo la Moshi mjini Mkoani Kilimanjaro leo.
 Wananchi wakishangilia kwa furaha wakati mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani, alipohutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro leo.
 Mwananchi akishangilia kwa nguvu zake zote, mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani, alipohutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya CCM Majengo, jimbo la Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro leo.
 Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni
 Wananchi wakijimwayamwaya Uwanjani wakati wa mkutano huo
 Wananchi wenye mkutano huo wakinyoosha mikono kuahidi kuwachagua wagombea wa CCM, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu, tangu mgombea wa Urais, Dk John Magufuli, Wabunge na madiwani
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akishiriki kucheza ngoma, wakati kikundi cha kina mama kutoka Moshi Mjini kilipotumbuiza wakati wa mkutano huo
 Mgombea Mwenza wa urais kwa tiketi ya CM, Mama Samia Suluhu akiwafurahia wananchi waliokuwa wakiselebuka mbele yake kwa furaha wakati wa mkutano huo.
 Vijana wakitoa burudani wakati wa mkutano huo
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM akimshukuru Mzee, Omari Mwariko (65) , baada ya mzee huyo kumkabidhi zawadi ya picha za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Kawawa , wakati wa mkutano huo
 Mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, akizitazama vema picha alizokabidhiwa na mchoraji huyo, Mzee, Mwariko
 Kamanda wa Umoja wa Vijana, Kinondoni Dar es Salaam, Angela Kairuki, akishauriana jambo na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, wakati wa mkutano huo wa kampeni
 Mgombea Ubunge jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya CCM,  Devis Mosha akimwaga sera wakati wa mkutano huo
 Mama Samia, akimpongeza Devis Mosha kwa hotuba nzuri
 Mbunge wa kuteuliwa, mkoa wa Tanga, Ummy Mwalimu, akiwaombea kura wagombea wa CCM, Dk. John Magufuli kwa upande wa Urais na wabunge na madiwani, wakati wa mkutano huo.
 Aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la Nkenge, mkoani Kagera, Asupta Mshanga, akiwaasa wananchi kuacha kuhama vyama baada ya kukosa nafasi za uongozi wanazoomba, alipohutubia mkutano huo, akisema " Mbona mimi licha ya kuwa ni mwanamke, baada ya kukosa nafasi ya kugombea ubunge kutokana na kura kutotosha nimetulia ndani ya Chama changu? Lakini wanaume wazima tena wengine wazee, wamekosa nafasi eti wanahama!"
 Mbunge wa Afrika Mashariki Angela Kizigha akizungumza, kumkaribisha mgombea Mwenza, Mama Samia kuzungumza, wakati wa mkutano huo. Katikati ni Katibu Mkuu wa UWT Amina makilagi
 Mgombea mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia akiwanadi wagombea wa Ubunge, Davis Mosha (Moshi Mjini), Innocent Meleck (Vunjo) na Dk. Siril Chami (Moshi Vijijini) wakati wa mkutano huo.
Wadau wakifuatilia hali ya mambo wakati wa mkutano huo. (Picha zote na Bashir Nkoromo,

MGOMBEA MWENZA WA URAIS MAMA SAMIA SULUH HASSAN ALIVYOPOKEWA MKOA WA KILIMANJARO,AIZITEKA WILAYA ZA TARAKEA,VUNJO NA MOSHI MJINI, ATAJA KIPAUMBELE ATAKAPOKUWA MAKAMU WA RAIS ASEMA ATAHAKIKISHA VIFO VYA KINA MAMA NA WATOTO VINAENDELEA KUPUNGUA KWA KASI, ATEMBELEA PIA HOSPITALI ZA UHURU..

 Wananchi wakiwa wanamsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais Samia Suluh Hassan wakati alipokuwa akiwahutubia Moshi Mjini




 Mgombea Mwenza wa Urais Samia Suluh Hassan akihutubia


TARAKEA NA RONGAI-ROMBO

Mgombea mwenza kwa tiketi ya Chama cha mapinduzi CCM,Samia Suluh Hassan ,amesema kuwa Serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya kikwete imefamefanya kazi kubwa katika sekta ya afya hususani kudhibiti vifo vya kina mama na watoto.


Bi samia ambaye yupo mkoani Kilimanjaro akiendelea na kampeni za urais akiwa ni  mgombea mwenza wa wa Mgombea Urais John pombe Magufuli mesema hayo baada ya kutembelea hospitali ya Huruma , iliyopo jimbo la Rombo, ambapo amesema kuwa hata wao watakapoingia Seikalini watahakikisha wanatekeleza kwa yale yaliyoachwa na serikali ya awamu ya nne, yakuhakikisha vifo vya mama na mtoto inakuwa historia kwa kuwa wataboresha sehemu za afya.


Katika hospitali ya Huruma , bi Samia pia alitembelea wodi za kinamama, na kuwapa pole, huku akihaidi kuwa Serikali inayokuja ya awamu ya tano itakuwa ya CCM, hivyo wasihofu waendelee kumuunga mkono kama mama jasiri aliyepata nafasi ya kuwawakilisha wanawake katika ngazi kubwa ya umakamu wa rais.


Baadae Bi Samia akaendelea na safari ambapo alifika Rongai na Tarakea, katika jimbo hili la Rombo na kuzungumza na wananchi, huku akiwahaidi vijana kuwapa kipaumbele katika kuwapa mitaji ili wajikombo katika umasikini.


MGOMBEA URAIS JOHN POMBE MAGUFULI AFUNIKA KATAVI PINDA ASEMA CCM HAIJAKOSEA KUMTEUA KUPEPERUSHA BENDERA YA CCM

 Mgombea Urais wa CCM JOHN POMBE MAGUFULI akiwahutubia wananchi wa Katavi

Sunday 23 August 2015

JK AFUNGUA KAMPENI ZA CCM, ASEMA WAGOMBEA WA UPINZANI NI WADHARURA TU, CCM ITASHINDA KWA KISHINDO





MGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM JOHN POMBE MAGUFULI AFUNIKA JANGWANI, AFUNGUA KAMPENI RASMI





 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube