BREAKING

Tuesday 18 August 2015

KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CHAMA CHA CCM, TAIFA YATANGAZA WAJUMBE WA KAMATI YA KAMPENI YA CHAMA HICHO, KINANA NI MWENYEKITI.



    NAPE NNAUYE Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa.
 NAPE NNAUYE Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa,wakti akizungumza na waandishi wa habari

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapindizi CCM, Taifa ambayo iliketi katika kikao chake cha jana,Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini Dar es Salaam, chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete,imemekamilisha kazi ya uteuzi wa wagombea Ubunge katika majimbo mawili ya Singida Mashariki na Kiteto

Akizungumza na waandishi wa habari Lumumba Jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi NEC Nape Nnauye, amesema kuwa wagombea Ubunge walioteuliwa kupeperusha bendera ya CCM, katika majimbo hayo  ni pamoja na Jonathan Njau Singida Mashariki,na Emmanuel Papian John ambaye atapeperusha bendera ya jimbo la Kiteto.

Nape amesema kuwa kamati hiyo imezingatia mambo mbalimbali katika kuteua wagombea hao katika majimbo hayo, kwa lengo la kupata uongozi bora.

Aidha Nape amesema kamati hiyo imefanya uteuzi wa Kamati ya wajumbe 32 wa kampeni, kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu ambayo itaongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Bwana Abdulrhaman Kinana, ambapo pia imewajumuisha baadhi ya wajumbe ambao walikuwa wagombea urais kupitia tikekti ya CCM, akiwepo Waziri wa Mambo ya Nje Bernad Membe, Januari

Makamba,Mwigulu Nchemba, Stephen Wasira,Razaro Nyalandu, na Makongoro Nyerere, wengine ni  Vuai Ali Vuai kutoka Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha Zanzibar, na Seif Khatib.


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube