BREAKING

Saturday, 1 March 2025

ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.


Mwimbaji nguli wa Muziki wa Injili Afrika Mashariki na Kati, Rose Mhando amesema amekiri kwamba Mkurugenzi wa Msama Promotions ambaye ni mwandaaji  wa matamasha mbalimbali ya Muziki wa Injili  Alex Msama,  ni zaidi ya Baba kwake kwani tangu alipoanza kazi zake za Uimbaji wa nyimbo za  Injili amekuwa akifanya naye kazi kwa wema bila dhuluma na Msama hajawahi nidhulumu. 


 Muhando alisema yeye pamoja na baadhi ya wasanii wenzake wa muziki wa Injili, hawawezi kujivunia mafanikio yao bila kutaja jina la Alex Msama ambaye hivi karibuni alipata tuzo ya Muandaaji Bora wa Muziki wa Injili wa wakati wote

Rose ametoa  kauli hiyo baada ya hivi karibuni kuwapo  taarifa kwenye mitandao ya kijamii, zikidai msanii  huyo aliwahi kudhulumiwa haki zake na Msama.

Akizungumzia kuhusu madai hayo, Rose alisema ameshitushwa sana na kusikitishwa sana na tarifa hizo na kuongeza kuwa hajui zimetokea wapi na watunzi wa uzushi  huo wana lengo gani.

Alisema katika maisha yake  mafanikio yake ya muziki huo, Malkia huyo wa Muziki wa Injili alisema hawezi kumsahau na kutaja jina la Msama ambaye ametumia muda mwingi wa maisha yake na fedha zake kuibua na kukuza na kulea vipaji wa vya muziki wa Injili na kuhakikisha haki zao zinalindwa.

Akitolea mfano,  Rose anasema Msama alikuwa ananisaidia kutoa ushauri wakati wa kuandaa muziki, alitoa msaada mkubwa wa fedha kuingia studio na kurekodi na zaidi ya yote alianzisha vita ya kukabiliana na wahuni waliokuwa wakiiba na wakiuza cd zetu na kuwafanya wasanii hao kukosa haki zao na kuishi maisha ya shida. 

"Kwangu mimi, Msama ni zaidi ya Baba, amenisaidia  mambo mengi sana, kuanzia fedha hadi ushauri, amenivumilia hata ninapomkwaza , leo mtu anaweza kuchapisha taarifa na kueleza kwamba eti Msama aliwahi kunidhulumu, hii sio kweli kabisa sjawahi na siwezi kusema kauli hiyo dhidi ya Msama, alisisitiza Rose Muhando. 

Alisema kuwa "yapo mambo madogo ya kibinadamu yaliyowahi kutokea wakati wa kazi, ikiwamo mimi mwenyewe kumkwaza Msama, lakini hiyo haina maana kwamba Msama amewahi kunidhulumu haki zangu 
Kwa mujibu wa Rose, ataendelea kufanya kazi na Msama wakati wowote atakapohitajika na ataendelea kuwa chini yake kwani anaamini mfanyabiashara huyo anamapezi ya dhati ya muziki wa Injili toka moyoni na Serikali inapaswa kumuangalia kwa jicho tofauti na hata kumpa msaada. 

" Mimi na baadhi ya wasanii wenzangu tulifika hatua ya kumuita Msama kuwa ni Askofu wa Muziki wa Injili, yule Baba ana mapenzi na muziki wa Injili toka moyoni, ni mtumishi wa Mungu aliyeamua kufanya utumishi wake kwa kukuza vipaji vya wasanii wa muziki huo.

Alimwomba Mh Rais Samia Suluhu Hassan kumuangalia Msama na kumlinda pale anaponyanyaswa na baadhi ya watendaji wa Serikali kwani kumuua Msama ni kuuwa ndoto na maisha ya wasanii wa Muziki wa Injili.

Kuhusu hatma yake kwenye muziki huo, Rose alisema muda mrefu alijiweka kando kutokana na changamoto za kiafya, lakini hivi sasa anaandaa Albamu mpya ya muziki wake ambayo itazinduliwa wakati wowote mwaka huu.

"Baada ya kutoka hospitali, nilijipa muda wa kupumzika, lakini hivi sasa naandaa Albamu yangu ya kukata na shoka, itazinduliwa wakati wowote mwaka huu na itakapokuwa tayari nitawajulisha washabiki wangu," 

 

Friday, 21 February 2025

UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA








Katika kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita  za kuboresha huduma za afya nchini  Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imenza kambi maalum ya upasuaji wa upandikizaji wa meno bandia kwa njia ya kisasa kwa wagonjwa ambao wamepoteza meno yao kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kambi hiyo Daktari Bingwa wa Afya ya Kinywa na Meno MNH.Mloganzila Dkt. Peter Shempemba  amesema wagonjwa watakao hudumiwa katika kambi hiyo ni pamoja na wale ambao walifanyiwa upasuaji mwishoni mwa mwaka jana na wale ambao wanakuja  kwa mara ya kwanza.

Ameongeza kuwa kundi la kwanza ni wale  ambao walishawapandikiza mizizi ya meno katika awamu ya kwanza na kipindi hiki watapandikizwa meno na kundi lingine  ni wale ambao wanapandikizwa mizizi kwa mara ya kwanza.

“Upandikizaji huu ni wa ubora wa hali ya juu, meno tunayoyapandikiza hayana tofauti na meno ya asili kwakuwa yanapandikizwa moja kwa moja kwenye mfupa wa taya na yanadumu kwa   muda mrefu, hayawezi kutoka kirahisi, mtu ataweza kutafuna vizuri kama kawaida ” amesema Dkt. Shempemba.

Kambi hiyo inafanyika kwa kushirikiana wataalam wa ndani na Daktari Bingwa aliyebobea katika Upasuaji wa Taya kutoka Hospitali za Wochhardt Dkt. Chirag Desai ambapo itafanyika kwa kipindiki hiki cha siku saba kuanzia tarehe 20 hadi 26 Februari, 2025 ambapo takribani wagonjwa 45 watafanyiwa upandikizaji.

Thursday, 13 February 2025

UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akiwasili katika viunga vya wa Shuele ya HolyLand Pre-&Primary School ikiwa ni ziara ya Maendeleo ya Elimu, Kulia ni Mmliki wa Shule hiyo Lawena Nsonda (Baba Mzazi EeBaba)

 



Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembelea, Shule ya Holy Land Pre-and Primary School iliyopo Wilayani Chunya, kushoto ni Mmiliki wa Shule hiyo Lawena Nsonda (Baba Mzazi)


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera akiteta jambo na Mmiliki wa Shuele ya HolyLand Pre-&Primary School Lawena Nsonda Baba Mzazi.


Baadhi ya Wanafunzi wa wa Shuele ya HolyLand Pre-&Primary School wakimlaki Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera



 

Tuesday, 4 February 2025

MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI


Mkurugenzi wa Msama Promotions ndg Alex Msama Amewaonya waimbaji wote wa nyimbo za injili Ambao wamekuwa wakishiriki kwenye majukwaa na wasanii muziki wa kidunia, kwani kufanya ivo ni kushiriki kwenye kumtukuza shetani.

Pia amewataka wasanii hao kuacha tamaa ya pesa ambayo inawapelekea wasanii hao kwenda kushiriki kwenye majukwaa ya muziki wa kidunia,

“Nawaonya waache kushiriki madhabahu za shetani,2 Wakorinto 6: 14-18 Msiambatane pamoja na watu wasioamini, pia wajihadhari na kupenda pesa kwani pesa nyingine ni za maagano ya kuzimu” Alex MSAma

Alex Msama ni mdau mkubwa wa Muziki wa Injili na Hivi karibuni alipokea tuzo ya heshima ya kuwa muandaaji bora wa matamasha ya injili nchini Tanzania ambayo maarufu yalikuwa yanafahamika kwa jina la TAMASHA LA PASAKA

Friday, 10 January 2025

DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA




Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeeleza kuridhishwa na oparesheni zilizofanyika mwaka jana 2024 kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola ambapo ilifanikiwa kukamata dawa za kulevya Kilogramu 673.2 za Methamphetamine na heroin, miongoni mwa hizo, kilogram 448.3 ziliwahusisha raia wanane wa Pakistani.

Kamishna Jenerali wa Mamlaka hiyo Aretas Lyimo amesema sehemu kubwa ya dawa hizo zikikamatwa katika bahari ya Hindi katika harakati za kuingizwa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari amesema Serikali ya awamu ya sita kuputia mamlaka ya kudhibiti Dawa za Kulevya DCEA kwa mwaka 2024 ilifanya mapinduzi makubwa katika kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya na kwamba katika dawa zilizokamatwa zipo zilizokutwa zimefichwa ndani ya jahazi la raia hao wa Pakistan.

Aidha katika hatua nyingine Kamishna huyo amesema Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kuhakikisha inaikinga jamii dhidi ya Madhara yatokanayo na dawa za kulevya akieleza pia jinsi watumiaji wanavyotumia vibaya bahari ya Hindi kufikisha madawa hayo nchini.

NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO



 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt Doto Biteko amekerwa na utendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akitoa maagizo uongozi wa kituo cha miito ya simu (call centre) ufumuliwe.


Maagizo ya Dk Biteko kwa Tenesco ni kufuatia kutotekelezwa kwa maagizo yake ya aliyoyatoa mwaka jana ya kuwepo kwa namba ya mawasiliano ya wateja isiyolipiwa ambapo itamwezesha mteja kupiga simu bila kukatwa salio  agizo ambalo halijatekelezwa.

Dkt Biteko ameyatoa maagizo hayo  baada ya kutembelea kituo cha miito ya simu Tanesco ambapo amesema watendaji wa shirika hilo wamezoea kazi.



Saturday, 20 July 2024

MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping katika ukumbi wa The Great Hall of the People kabla ya kuanza mazungumzo jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na ujumbe wake wakiwa kwenye kikao cha pamoja na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping na ujumbe wake katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.






 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube