BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Sunday, April 06, 2025

Monday, 17 August 2015

KUONDOKA KWA MAKADA WA CCM, KINANA, MAGUFULI, NAPE BADO WANAMTAJI KISIASA, NA MVUTO.....


Wimbi kubwa la baadhi ya wanachama na makanda kuhamia chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, ama ule muungano wa UKAWA, bado si tishio kwa Chama cha CCM, kutokana na mtaji walionao wa wanachama wao.

Nimefanikiwa kuzunguka Tanzania nzima nikiwa na dhamira nzuri yenye matunda kwangu, lakini kubwa nimefanikiwa kuambatana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Ndugu Abdulrhaman Kinana, ambaye amezunguka nchi nzima kukagua ahadi za Uchaguzi Mkuu za Mwaka 2010, akiangalia utekelezaji wake, safari ambayo imetumika kwa miaka miwili,amekagua, amejenga, amesaidia japo penye kutoa msaada hakupenda aandikwe kwa kuwa ni jukumu lake binafsi.

Sikumshangaa sana, kwa kuwa tayari nilishamuzoea kwa kuwa tangu alipochaguliwa kuwa katibu Mkuu wa CCM, safari yake ya kujitambulisha ya kwanza kabisa ilikuwa ni Mkoa wa Mtwara, akiambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa, Ndugu Nape Nnauye, ambaye Kinana mara nyingi humwita kiboko ya wapinzani, na hapo alionyesha kuwa anaweza kumsaidia mtu yoyote na asitake kusifiwa wala mkono wa kulia usifahamu alichotoa ni nini, huu ni mfano wa kuigwa kwa kuwa pia huyu ni Muumini mzuri wa dini ya Kiislamu, yenye maadili ya Heyeya (UTUKUFU)

Sitaki kumsifia sana na wala sitaki kuzungumza mengi ambayo nimekutana nayo nikiwa mmoja wa wandishi waliokuwa katika uso wake kumtafakari, ila hapa naeleza jinsi siasa ya Chama cha mapinduzi ilivyo kwa sasa, kuondokewa na wanachama ni juhudi za kupata wanachama wapya, na pengine siasa tunazoziona sasa ni zile za mjini tu tukienda Vijijini utakutana na umati mkubwa wenye nguo za Kijanani, hivyo Kinana na Nape wametengeneza wanachama wapya kwa staili ya kipekee Mikoani, na hata hawajatumia nguvu kubwa pengine hii tunaweza kuiita 'KUONDOKA KWA MAKADA WA CCM, KINANA, MAGUFULI, NAPE BADO WANAMTAJI KISIASA, NA MVUTO.....''

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube