BREAKING

Kimataifa

 


UMRI WA KUJIUNGA NA JESHI UKRAINE WAPUNGUZWA

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametia saini kuwa sheria mswada wa kupunguza umri wa wanaosajiliwa kuingia jeshini kwa miaka miwili kutoka 27 hadi 25.

Kyiv imekabiliwa na hasara kubwa vitani baada ya miaka miwili ya vita, ambapo Urusi imenufaika kutokana na kuwa na wanajeshi wengi.

Hatua hiyo itairuhusu Ukraine kusajili watu wengi ili kuwa na wanajeshi wengi wa akiba, baada ya idadi ya waliojitolea kupungua.

Bw Zelensky alisema mnamo Desemba kwamba wanajeshi 500,000 zaidi walihitajika.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube