BREAKING

Saturday, 8 November 2025

BAADA YA KUJIONDOA KUGOMBEA NAFASI YA SPIKA KADA WA CCM ALEX MSAMA ASEMA DKT .TULIA NI MKOMAVU WA KISIASA...


Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mkurugenzi wa Msama Promotion Ndugu Alex Msama amesema ameona Watanzania wengi wakikosoa au kulaumu kitendo cha Dkt. Tulia Ackson kujiondoa kwenye michuano wa kugombea Uspika wa Bunge kwamba labda kuna kitu kibaya, au hatakiwi au amesusa.

Msama amesema kujitoa kwa Dkt. Tulia ni jambo zuri linaloashilia ukomavu wake wa kiuongozi na Kidemokrasia, amesema Dkt. Tulia hana kashfa mbaya, sio fisadi, sio mla rushwa bali ameonesha kwa vitendo ubora wake katika Uongozi hadi kuchaguliwa kuwa Rais wa Wabunge wote Duniani.

"Amewaachia nafasi wengine waweze kupata baada ya yeye kufanya vizuri katika kipindi chake, inaonesha hana tamaa na madaraka, na kwa uwezo wake mkubwa ni matumaini yangu kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan atamteua katika nafasi nyingine kubwa ili andelee kuwatumikia Watanzania' - amesema Msama.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube