BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Thursday, April 10, 2025

Thursday, 12 April 2018

RAIS MAGUFULI AMSIFU RAIS MSTAAFU AWAMU YA NNE JAKAYA KIKWETE BAADA YA UZINDUZI WA TAASISI YA JAKAYA MRISHO KIKWETE FOUNDATION


Rais  Dkt.John Pombe Magufuli­­ amemwagia sifa kemkem Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, wakati wa uzinduzi wa taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF), Ikulu jijini Dar es Salaam.
Dkt. Magufulu alisema, Rais mstaafu Kikete, amefanya mambo mengi makubwa nchini, katika nyadhifa mbalimbali alizoshikaserikalini na kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Mheshimiwa Kikwete, umefanya mambo makubwa kwa faida ya nchi yetu, katika nafasi mbalimbali ulizoshika ikiwemo kwenye chama, Jeshini, na hata ulipokuwa Rais, kwakweli unastahili pongezi nyingi”Alisema Rais Mahgufuli katika hotuba yake.
Alisema, Dkt. Kikwete ameimarisha uchumi wa nchi, kujenga demokrasia lakini pia kujenga mahusiano mema na nchi za nje.
“Hata mimi urais wangu kwa miasi kikubwa umetokana na msimamo wako, kwakweli ulinibeba na mimi nitakubeba sintakuangusha” alisema.
Awali akielezea madhumuni ya taaisi hiyo, iliyoanzishwa Februari mwaka 2017, Dkt. Kikwete ambaye ndiye mwenyekiti, alisema, ni pamoja na kuleta mageuzi katika maisha ya watu hapa nchini Tanzania na kwingineko katika Afrika kwa kutoa majawabu yenye ubunifu, ya kweli kweli na endelevu kwa changamoto zinazowakabili wananchi
“Lakini pia dhima ya taaisi ni kushirikiana na serikali na wadau wengine katika kuleta mageuzi ya kimaendeleo katika katika ubora wa maisha ya watu katika Tanzania na kwingienko.” Alisema Dkt. Kikwete.
Akieleza zaidi Rais huyo mstaafu alisema, taaisi hiyo inalenga kufanya kazi katika Tanzania na Bara la Afrika (Pan Africa).























 




No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube