BREAKING

Thursday 12 April 2018

KAMBALE AWA KIBOKO KWA YANGA



Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Young Africans wameshindwa kutamba katika Uwanja wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Singida United jioni hii.

Singida United ndiyo walikuwa wa kwanza kupachika bao katika dakika ya pili tu ya mchezo kupitia kwa Kambale Salita.

Zikiwa zimeongezwa dakika 3 kuelekea mapumziko, Yanga walisawazisha bao hilo kupitia mpira wa adhabu ya kona uliopigwa na Ibrahim Ajibu na kumkuta beki Abdallah Shaibu ambaye bila ajizi aliutia kimiani kwa kichwa.

Matokeo hayo yanakuwa yanaipa msala Yanga ambayo imerejesha tena pengo la utofauti wa alama 5 kati yake na Simba iliyo kileleni kwa kuwa na pointi 52.

Utofauti wa alama hizo unaiweka Yanga katika mazingira magumu ya mbio za kuwania ubingwa wa ligi kati yake na Simba ambayo ina njaa ya kutouchukua kwa takribani miaka mitano sasa. 

Sare hiyo imeifanya Yanga kujiongezea alama moja pekee kwa kufikisha 47, kwenye nafasi ya pili ya msimamo wa ligi.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube