BREAKING

Monday 27 February 2017

BARCELONA, MADRID WAKAMATANA JUU KWA JUU..LA LIGA

Lionel Messi akipongezwa na mchezaji mwenzake Neymar Jr













Sunday 26 February 2017

SIMBA NI ILE ILE NA MASHABIKI NI WALE ALEEEEEEE, YAITANDIKA YANGA BAO 2-1 NA KUJICHIMBIA KILELENI MWA LIGI

 Mshambuliaji wa Simba Laudit Mavugo akitafuta njia ya kumtoka Beki wa Yanga Kelvin Yondan

Beki wa Simba Janvier Besala Bukungu akichuana vikali na kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima.


Shuja wa Simba aliyefunga bao la Ushindi Shiza Ramadhan Kichuaya akiwa amenyanyuliwa na Menmeja wa Simba Mussa Hassan Mgosi, baada ya kufunga bao.


MBUNGE RITTA KABATI KUSAIDIA UJENZI WA OFISI TATU ZA CHAMA CHA MAPINDUZI MANISPAA YA IRINGA


MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akimkabidhi mifuko ya saruji kwa ajiri ya ujenzi wa jengo la ofisi ya chama katika kata ya Ruaha kwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza 
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa katika eneo la uwanja wa kujenga ofisi ya kata ya Ruaha 
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akibadilishana mawazo na katibu wa ccm manispaa ya Iringa Nuru Ngereja
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa hama hicho wa kata ya ruaha
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa na 
mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza pamoja na viongozi wengine wa chama hicho.
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati akipokelewa na wanachama wa mtaa wa kigamboni mkoani Iringa

Na Fredy Mgunda,Iringa.

MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) ameanza kusaidia Ujenzi wa ofisi za Matawi ya CCM katika kata mbali mbali za Jimbo la Iringa mjini kama sehemu ya majukumu yake ya kukijenga chama hicho ambacho kilipoteza kiti cha ubunge na halmashauri kuchukuliwa na wapinzani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mifuko ya saruji kwa Ujenzi wa ofisi za Tawi Kigamboni na Ruaha ,Kabati alisema kuwa anafanya hivyo kama njia ya kutekeleza ilani na maadhimio ya miaka arobaini ya chama cha mapinduzi.
“Nakipenda chama changu ndio maana napigana sana kuhakikisha chama cha mapinduzi mkaoni mhapa iringa kinarudi mahala pake na kuhakikisha kinaaminika kwa wananchi na wanachama wa  manispaa ya Iringa”.alisema Kabati 

Hata hivyo Kabati alisema kuwa ataendelea kusaidia Ujenzi wa ofisi hizo ili kuona ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu ama sita kila tawi linakuwa na ofisi yake ya tawi na aliwataka wanachama wa CCM kushikamana na kuendelea na Ujenzi wa ofisi hizo pamoja na kujihusisha na shughuli nyingine za kijamii

"Haiwezakani chama kikubwa kama hiki kukosa ofisi za matawi wakati tunamaeneo mengi ya kujenga ofisi nitakikisha tunashirikiana na wanachama na wananchi wengine kujenga hizo ofisi ili kumuunga mkono Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DR John Pombe Magufuli ambaye anapambana kuhakikisha cha mapinduzi kinakuwa chama cha wananchi wa chini na sio matajiri pekee yao".alisema Kabati

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza aliwataka wanachama kuwa kusahau yaliyopita na kuanza kujenga chama upya.
“Tulipoteza halmashauri ya Iringa na jimbo hivyo inabidi tukae chini na tujipange upya kukijenga chama maana tunajua kwa kujenga ofisi za matawi zitatusaidia kurudisha hadhi na hali ya chama hapa manispaa kwa kutoa huduma bora kwa wananchi wote bila kuchagua chama”.alisema Kiponza 

Kiponza alimshukuru mbunge wa viti maalumu Ritta kabati kwa mchango anaoutoa kwa kuleta maendeleo katika manispaa ya Iringa hasa ukiangalia ujenzi wa majengo mbalimbali ya shule,taasisi za kidini,taasisi za kijamii hapa kujenga majengo ya chama.

Lakini Kiponza alimtaka mbunge Kabati kuwasaidia wananchi wanaodhurumiwa na kunyang’anywa mali zao katika manispaa ya Iringa.

“Hapa kigamboni kunawananchi wanapigwa na viongozi wa mtaa kwa kuwa wapo CCM tu na wamenyang’anywa kituo cha kuchotea maji ambacho kilikuwa mradi wa chama cha mapinduzi hivyo lazima upambane kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na mali za chama zinarudi kwenye chama”.alisema Kiponza

 Naye Katibu wa CCM manispaa ya Iringa Nuru Ngeleja alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha ofisi zote za chama zinajengwa na zinakuwa katika ubora unaotakiwa kutokana na ukubwa wa chama cha mapinduzi(CCM) na kuahidi kuwa wataendelea kumuunga mkoano Rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania Dr John Pombe Magufuri.

“Sisi tunafanyakazi ya kumsaidia mwenyekiti wetu wa chama ambaye ni Rais wetu kwa kufanya kazi na kuisimamia serikali kufanya kazi kwa uhakika na kuwafaikia na kuwatumikia wananchi waliowaweka madarakani mpaka sasa”. Alisema Ngereja

Thursday 23 February 2017

SERIKALI YAAHIDI KUUNGA MKONO JITIHADA ZOTE ZINAZOFANYWA NA WADAU WA MICHEZO NCHINI ZENYE LENGO LA KUENDELEZA SOKA LA VIJANA

Waziri wa habari utamaduni sanaa na michezo Nape Nnauye akizungumza wakati wa Uzinduzi huo

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Nnauye akisisitiza jambo
Serikali imeahidi kuunga mkono jitihada zinazofanywa na wadau mbalimbali wa sekta ya michezo nchini, zenye lengo la kuendeleza soka la vijana na soka la wanawake nchini jambo litakalosaidia viwango vyake viendane na kasi ya ushindani kimataifa.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa habari utamaduni sanaa na michezo wakati wa uzinduzi wa bodi ya mfuko huru utakaokuwa maalum kwa maendeleo ya soka la vijana na soka la wanawake, utakaokuwa na jukumu la kubuni vyanzo mbalimbali vya rasilimali fedha kwa ajili ya maendeleo ya timu hizo za taifa.

Katika hatua nyingine waziri Nape amewaomba wajumbe wa bodi ya mfuko huo kutekeleza makujukumu yao kama ilivyoainishwa kwenye katiba yake, huku akiwasihi watanzania kuiunga mkono bodi hiyo, jambo alilosema litasaidia soka letu kupiga hatua kutoka hapa lilipo.

NAMAINGO BUSSINESS AGENCY NA NHIF YAWAKUTANISHA WAJASIRIAMALI WA MKOA WA TANGA


MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wajasiriamali  na Taasisi ya Kibiashara ya Namaingo Bussiness Agency uliokuwa na lengo la kuwahamasisha kujiunga na bima ya Afya na kuhalalisha biashara zao

JA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wajasiriamali  na Taasisi ya Kibiashara ya Namaingo Bussiness Agency uliokuwa na lengo la kuwahamasisha kujiunga na bima ya Afya na kuhalalisha biashara zao

MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wajasiriamali  na Taasisi ya Kibiashara ya Namaingo Bussiness Agency uliokuwa na lengo la kuwahamasisha kujiunga na bima ya Afya na kuhalalisha biashara zao
Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahima akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali wa wafanyabiashara na wajasiamali mkoani Tanga leo
Mkurugenzi wa Kampuni ya Namaingo Business Agency, Bi Ubwa Ibrahim akisisitiza jambo kwenye mkutano huo wa pamoja.
 Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Miraji Kisile akifafanua namna ya wajasiriamali na wafanyabiashara wanavyoweza kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo za matibabu kupitia mfuko huo 
  Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Miraji Kisile akifafanua namna ya wajasiriamali na wafanyabiashara wanavyoweza kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo za matibabu kupitia mfuko huo ikiwemo kufanya biashara zinazotambulika kisheria ili kuisaidia serikali kupata mapato
 Baadhi ya wafanyabiashara na wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali mkoani Tanga wakifuatilia mkutano huo


 Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Miraji Kisile akimsikiliza kwa umakini mmoja wa wafanyabishara waliojitokeza kwenye mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Police Mess mkoani Tanga
 Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Miraji Kisile akisistiza jambo katika mkutano huo kwa baadhi ya wafanyabiashara namna wanayoweza kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya kwa ajili ya kupata matibabu

 Baadhi ya wafanyabiashara na wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali mkoani Tanga wakifuatilia mkutano huo
Baadhi ya wafanyabiashara na wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali mkoani Tanga wakifuatilia mkutano huo Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

Wednesday 22 February 2017

NAPE KUZINDUA MFUKO WA KUSAIDIA SERENGETI BOYS

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Nape Nnauye 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Nape Nnauye kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa miguu kwa vijana na wanawake.

Uzinduzi huo utakaofanyika saa 5.00 asubuhi, utahudhuriwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Mkurugenzi wa Michezo, Yussuph Singo. Utafanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Courtyard, Upanga jijini Dar es Salaam.

ROGER FEDERER ASAINI MIAKA 3 KUCHEZA MASHINDANO YA NDANI USWISI






Roger Federa


Roger Federer amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kushiriki michuano inayofanyika mjini Basel nchini Uswisi kila mwaka.

Bingwa wa michuano ya tennis ya Australia kwa mwaka huu Roger Federer amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kushiriki michuano inayofanyika mjini Basel nchini Uswisi kila mwaka.

Kwa mujibu wa waandaji wa michuano hiyo kuongezeka idadi ya nyota wenye majina kunaipa michuano hiyo uzito.

Tangu aanze kushiriki michuano ya ndani kuanzia mwak 1998 Federer ameshinda mataji makubwa 7 ya kitaifa. 


Federer mwenye miaka 35 amerejea katika mashindano ya mchezo huo mwezi januari mwaka huu ikiwa ni baada ya kukaa kwa kipindi kirefu kufuatia majeruhi.

JUMA KASEJA BADO ANAKIMBIZA, ACHAGULIWA KIPA BORA MWEZI JANUARI....LIGI KUU BARA


Mlinda mlango mahiri wa timu ya Kagera Sugar Juma Kaseja amechaguliwa mchezaji bora wa mwezi Januri na kuisaidia timu yake kwa kushinda mechi tatu mfululizo na kuwashinda wachezaji wenzake Mbaraka Abeid kutoka Kagera na Jamali Mtegeta wa Toto Afrika 
Afisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF Alfredy Lucas amezungumzia jinsi nyota huyo alivyoibuka mchezaji bora.

Tuesday 21 February 2017

MAJALIWA AWASALIMIA WANANCHI WA BASHNET AKIWA KWENYE ZIARA ZAKE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Bashnet wilayani Mbulu wakati aliposimamakijijini hapo akitoka Mbulu kwenda Hanang Februari 21, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday 20 February 2017

SIMBA NA YANGA JUMAMOSI , SERIKALI YABORESHA CAMERA ZA CCTV ZA UWANJA WA TAIFA KUWABAINI WAHARIBIFU WA MIUNDOMBINU

Huu ndio muonekano wa Uwanja wa Taifa kupitia Camera za CCTV

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA MBULU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa michezo wa Mbulu mkoani Manyara, Februari 20, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube