BREAKING

Wednesday 30 June 2021

EURO 2020- UKRAINE HIYOOO ! ROBO FAINALI



 Michuano ya EURO 2020 imeendelea kutikisa katika hatua ya robo fainali ambapo katika mchezo wa hatua ya 16 bora Ukraine imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Sweden.

Nyota wa mchezo huo Oleksandr Zinchenko alifunga bao dakika ya 27 bao ambalo baadae ililisawazishwa na mchezaji Emil Forsberg.

Dakika 90 za mchezo wa kawaida ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.

Baadae ziliongezwa dakika 30 na nyota Artem Dovbyk alipachika bao dk 120 na kuifanya timu yake ya Taifa ya Ukraine kutinga hatua ya robo fainali.

Timu ya Sweden ilipata pigo baada ya mchezaji wao Marcus Danielson katika dakika ya 99 alionyeshwa kadi nyekundu na kuwafanya Sweden kumaliza mchezo huo wakiwa pungufu.


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube