BREAKING

Monday 22 May 2017

ARSENAL YASHINDWA KUFUZU KWA MARA YA KWANZA KWA MIAKA 20

















Arsenal ilishinndwa kufuzu kwa kombe la klabu bingwa barani ulaya,  kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 20 licha ya ushindi wake dhidi ya Everton wa mabao 3-1 katika siku ya mwisho ya mechi za Primia League.

Arsenal ilianza mechi vizuri ikiwa pointi moja nyuma ya Liverpool na walikuwa katika nafasi bora kuchukua nafasi yao wakati waliongoza mnamo dakika ya nane.

Lakini ukakamavu wa Liverpool uliiwezesha kusalia katika timu nne za kwanza baada ya kuwatandika Middlebrogh mabao 3-0.

Manchester City ilishika nafasi ya tatu baada ya kuinyuka Watfoird mabao 5-0.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube