BREAKING

Monday 29 May 2017

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA KOREA KUSINI, AHOJIWA NA CCTV YA CHINA, LEO

 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na Balozi wa Jamhuri ya Korea Kusini hapa nchini, Song Geum-Young  alipomkaribisha katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es salaam, leo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea Kusini hapa nchini, Song Geum-Young Katika mazungumzo yao, Katika mazungumzaa hayo, wamehimiza suala la kuboresha mahusiano baina ya Jamhuri ya Korea Kusini na Tanzania pamoja na kuzungumzia ushirikiano wa muda mrefu katika kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini
Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana akihojiwa na Mwanishi wa Kituo cha Televisheni cha China Central Television - CCTV kuhusu mafanikio ya kiuchumi ambayo China imeyafikia na hatua mbalimbali za maendeleo ambazo Tanzania inajifunza na kushirikiana na China ili kufanikiwa kufikia uchumi wa kati.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube