BREAKING

Tuesday 30 May 2017

MULTICHOICE TANZANIA YASHEREKEA SIKU YA AFRIKA




Kwa kipindi kizima cha mwezi wa 5 (Mei) wateja wa DStv wamekuwa wakifurahia zaidi vipindi  vyenye ubora na vya kusisimua  vya Kiafrika.
Huba, Jikoni na Marion, Mchikicho wa Pwani, Yahusu Tanzania, Kimbembe ni kati ya vipindi kutoka Tanzania vilivyo bamba mwezi huu ndani ya chaneli Maisha Magic Bongo (DStv 160)
Meneja Mahusiano Multichoice Tanzania, Johnson Mshana amesema, “Mwezi Mei kwetu tumeufanya kuwa mwezi maalum kwa ajili ya kutangaza na kujivunia  utajiri wetu  waafrika ikiwa ni pamoja na utamaduni na Sanaa na michezo
Hii ni moja ya sehemu ya ahadi ya  DStv kwa kutoa ushirikiano kwenye  sekta ya sanaa na burudani kwa kuendelea kusaidia Filamu za Afrika na kwa kuwekeza katika watu, mawazo na vipaji.
Ikiwa ni njia moja wapo ya kusheherekea mwezi huu wa Afrka, Wafanyakazi  wa Multichoice Tanzania waliamua kuvaa mavazi maalum ya Kiafrika na kuandaa chakula maalum cha kiafrika kwa wafanyakazi wote.
Haikuishia hapo, Multichoice Tanzania pia imeandaa zawadi maalum za Kiafrika kwa waandishi wa habari, ikiwa ni njia ya kuonyesha shukrani kwa waandishi na kudumisha Umoja na Uafrika wetu.
#AFRIKAYETU

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube