BREAKING

Monday 9 January 2017

NI VITA NA VISASI NUSU FAINALI YA MAPINDUZI,ZANZIBAR KATI YA SIMBA NA YANGA....


Mavugo

MAPINDUZI


Na Mwandishi wetu Scolastica -Zanzibar

Ni simba na Yanga Jumanne zitachuana katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la Mapinduzi, huko Visiwani Zanzibar kwenye Dimba la Aman.

Watani hao wa jadi watamenyana huk wakiwa na kumbukumbu ya sare ya kufungana mabao 1-1, katika mchezo wa Ligi Kuu Bara mzunguko wa kwanza.


simba imefika katika hatua hiyo baada ya kuifunga  Jang’ombe Boys, mabao 2-0 huku shujaa akiwana ni Mrundi Laudit Mavugo aliyefunga mabao yote.

Mchezo huo utafanyika Jumanne Saa 2:15 usiku Uwanja wa Amaan, Zanzibar katika Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar timu hizo zinakutana kutokana na Simba kuongoza katika kundi lake la  A kwa pointi zake 10, ikifuatiwa na Jang’ombe Boys,huku Yanga wao wakishika nafasi ya pili katika kundi lake,lililoongozwa na Azam FC.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube