BREAKING

Thursday 30 July 2015

EDWARD LOWASSA KUCHUKUA FOMU LEO YA URAIS KUPEPERUSHA BENDERA YA CHADEMA

Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa pamoja na Mkewe Regina Lowasa wakiwa wakionyesha  kadi zao baada ya kujiunga na Chama cha Demeokrasia na Maendeleo CHADEMA.


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa leo  anatarajiwa kuchukua fomu kwa ajili ya kuomba ridhaa ya wanachama wa Chadema kupeperusha bendera ya chama hicho kwa nafasi ya Urais.

Bw. Lowasa ambaye ameleta hamasa mpya katika siasa za Tanzania kutokana na uamuzi wake wa kuhamia chama cha upinzani, anatarajiwa kufika saa tano makao makuu ya chadema kwa ajili ya kuchukua fomu ya urais.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusiana na taarifa zilizoenea kwenye baadhi ya mitandao kuwa watendaji wakuu wa chadema inasadikiwa wamehama chama hicho kupinga uamuzi wa kumpokea Lowasa, Salum Mwalimu amefafanua kuwa Lowasa leo atachukua fomu hiyo

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube