BREAKING

Monday 17 July 2017

CHAMA CHA RIADHA TANZANIA RT CHATANGAZA KUHAIRISHA MASHINDANO YA TAIFA KUFUTIA UKATA WA FEDHA.

WILHELM  GIDABUDAY-Katibu Mkuu wa RT


Katibu Mkuu wa Chama caha Riadha tanzania RT Wilhelm GidaBuday amesema kuwa kufuatia ukata wafedha wanaokabiliana nao wameamua kustisha mashaindano ya Taifa ambayo yalitakiwa kuanza kutimua vumbi Kibaha Mkani Pwani Julai 22 mwaka hu.

Gidabuday amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari akisema kufutia mwingiliano wa mashindano makubwa duniani yakiwepo mashindano ya dunia yanayofanyika hivi karibuni Uingereza pamoja na yale Bahamas, ambapo tayari wanariadha wamesafiri kuiwakilisha Tanzania, pamoja na yale ya Jamaica

Ameema kufuatia mwingiliano huo wameona ni vyema kuhairisha mashindano hayo ya Taifa hadi hapo yatakapotangazwa kwa mara nyingingi, huku akiwasihi wanariadha kuendelea kujifua zaidi.

Tayari baadhi ya wachezaji channel ten imewashuhudia wakijifua katika uwanja wa Taifa kujiandaa na mshindano ya Taifa ambayo yalikuwa yaanze Julai 22, lakini kuhairishwa kwa mashindano hayo sasa wanariadha hao watarejea katika vituo vyao.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube