BREAKING

Monday 17 July 2017

MSAJILI WA VYAMA VYA MICHEZO AWAKANA WAZEE WA KLABU YA SOKA YA SIMBA JUU YA KATIBA..

Ibrahim Sapi Mkwawa,Msajili wa Michezo 
Siku Chache tangu wazee wa klabvu ya soka ya Simba kuibuka kwa kumuomba Rais John Pombe Magufuli kuingilia katika maamuzi mabovu ndani ya klabu ya soka ya simba ikiwepo kufanya marekebisho ya katiba bila mkutano mkuu pamoja na kutosomewa baadhi ya mapato na matumizi hatimaye msajili wa Vyama vya Michezo ameibuka na kutoa ufafanuzi juu ya madai hayo.

Akizungumza na mtandao wa Shamakala360 ofisini  kwake Msajili wa Michezo Ibrahim Sapi Mkwawa, amesema kuwa madai hayo amekuwa akiyasikia kwenye vyombo vya habari, ambapo ameamua kusema taarifa sahihi juu ya yeye kupitisha katiba ya marekebisho kwani alichofanya ni kuhariri na kupunguza baadhi ya vifungu vya katiba ambavyo vilikuwa vinajirudia rudi.

Amesema kuwa hakuna katiba mpya iliyopelekwa kwake bali alifikishiwa katiba ya Simba kuihariri ambapo pale alipona kuna mapungufu aliirejesha kwa viongozi wa Simba ili kupunguza mapungufu aliyoyaona.

Aidha ameenda mbali kwa kusema baadhi ya mambo ambayo yalikosewa ndio yaliyomfanya kuwarejeshea viongozi wa Simba Katiba ili ifanyiwe uhariri tena, ambapo pia amesema malalamiko hayo.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube