BREAKING

Monday 17 July 2017

VITA YA WEZI WA KAZI ZA WASANII,MSAMA AJITOSA TENA


MSAMA-Mkurugenzi wa Msama Auction Mart.
Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart, inatarajia kuanza kuwakamata wezi wote wanaojishughulisha na wizi wa kazi za wasanii, ambapo itaanza kazi hiyo Jumatatu ya wiki inayokuja.

Kampuni hiyo kepitia Mkurugenzi wake Alex Msama imesema inaungana na Serikali kuhakikisha wezi  wa kazi za wasanii sasa inakuwa vita kwani wasanii wengi wamekuwa wakidhulumiwa kwa kiasi kikubwa.

Akizungumzia sula hilo Mkurugezi wa Msama Promosheni amesema kuwa watakaohusika katika zoezi hilo la kuwakamata ni pamoja na wale wanadurufu CD feki, pamoja na wale wanaonyonya nyimbo kwa kutumia kompyuta .

Amesema kuna vijana wengi wanafanya kazi hiyo na kurudisha nyuma maendeleo ya wasanii, ambao wamekuwa wakilia kila kukicha juu ya wizi huo.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube