BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Tuesday, 15 November 2016

SERIKALI YAKABIDHI BENDERA KWA MWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA KUMSAKA MREMBO WA AFRIKA YATAKAYOFANYIKA NOVEMBA 26 NCHINI NIGERIA


Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape nnauye, amemkabidhi bendera ya taifa mrembo,Julitha Kabete kwa ajili ya kwenda kushiriki shindano la Miss Afrika mjini Calabar nchini Nigeria ambalo litafanyika Novemba 26 Mwaka huu.

Waziri Nape amekabidhi bendera hiyo huku akitoa nasaha kwa mrembo huyo kuwa na nidhamu katika shindano hilo ambalo ni kwa mara ya kwanza kufanyika, ambapo pia ametumia muda huo kumweleza kwamba Serikali ipo bega kwa bega na ushiriki wake kwani kwa sasa Serikali inatumia mashindano kama hayo kutangaza sanaa zaidi.

Aidha Waziri huyo amesema kuwa wanathamini warembo kwa kuwa wamekuwa wakitangza Tanzani kupitia shindano hilo ambalo kidunia lina umaarufu mkubwa hivyo watanzania wanapaswa kumpigia kura nyingi mrembo huyo, huku Julietha akisema kuwa atatumia vyema ushindani wake kwani iwapo atashinda atakuwa ameitangza kwa kiasi kikubwa Tanzania kupitia sanaa ya Urembo.

Kauli ambayo imeenda sambamba na ya Mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga, kuwa katika mashindano hayo mrembo atakayepatikana atakuwa mwakilishi wa utunzaji wa Mazingira kufutia mabadiliko ya Tabia nchi.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube