BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Tuesday, 8 November 2016

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA AZAM FC MAREHEMU SAID MOHMED AZIKWA LEO MAKABURI YA KISUTU TENGA AMWELEZEA KWA UNDANI.




Rais wa zamani wa shirikisho la Soka Tanzania 'TFF'  na aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga amemwelezea aliyekuwa Mwenyekiti wa Azam FC, Sheikh Said Muhammad Abeid aliyefariki dunia jana jioni  katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, kuwa alikuwa mpenda michezo na asiyekuwa na maneno ya kukatisha tamaa.

Tenga ameeleza hayo wakati wa mazishi yake yaliyofanyika katika Makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, ambapo amesema katika vikao vyote ambavyo alikuwa akiingia juu ya kujadili mstakabali wa vilabu alikuwa kiongozi na mwenye kutatua matatizo ya vilabu hususani pale lilipokuja suala la Bodi ya Ligi kwa kuwa alikuwa anahusika kwa kiasi kikubwa.

Amesema kuwa Marehemu mzee said ambaye pia hadi mauti yanamkuta alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu, atakumbukwa zaidi na wadau wa soka kwa kuwa alikuwa mmoja wa watu waliobua vipaji vya soka kwa kuandaa mashindano mbalimbali yakiwepo ya Uhai.

Naye rais wa TFF Jamal Malinzi amesema kuwa katika Shirikisho lake amepoteza mtu mhimu ambaye alikuwa nguzo kubwa ndani ya TFF aliyekubali kukaa na watu wa rika lolote kwa ajili ya kujadili masuala ya soka , huku akimkumbuka kwa kuwa mmoja wa watu waliounganisha TFF na Azam kupta udhamini wa timu za vijana ikiwepo timu ya Taifa ya Vijana.




No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube