BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Tuesday, April 08, 2025

Wednesday, 9 November 2016

MWANASOKA ATHUR MWAMBETE ANAHITAJI MSAADA WA HALI NA MALI ,ALAZWA TASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE, WADAU WA SOKA CHONDE CHONDE OKOENI MAISHA YAKE....


Ezi za Mwambete akiwa na miguu yake kabla ya Mguu mmoja kukatwa


Aliyekaa kitandani ni msukuma Kandanda wa zamani Athur Mwambete, na pembeni yake ni madaktari bingwa wanaomhudumia wakiongozwa  na Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Professa Mohamed Janabi.

Na Said Makala

Wadau wa michezo kote nchini wameombwa kujitokeza kumsaidia mwana michezo Athur Mwambeta aliyelazwa katika taasisi ya magonjwa ya moyo ya Muhimbili.

Msaada mkubwa zaidi anaohitaji ni pesa ya kununulia miguu ya bandia.

Mtandao wako wa Shamakala360 ulimtembelea Athur na nikufanya naye mazungumzo, 

Msomaji umuonaye hapo ni mchezaji wa zamani wa timu za soka za Sunderland na Simba, Athur Mwambeta ambaye jina lake kamwe si geni masikioni mwa familia ya wapenda michezo kutokana na umahiri wake katika kusakata kabumbu kuanzia miaka ya sitini na sabini.

Lakini tunavyozungumza hivi sasa hali yake si nzuri na amelazwa katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika hospitali ya taifa ya muhimbili jijini Dar es Salaam kufuatia maradhi ya miguu kuuma sana.

Mwambeta ambaye sasa anakabiliana na maradhi hayo kwa mara ya pili baada kuwa na hali katika cha hivi karibuni jambo lililopelekea kukatwa mguu wa mmoja.

Na i hivi sasa kufuatia athari katika mguu uliosalia kuendelea kuwa kubwa kuna uwezekano akapoteza tena mguu mwingine.

Hospitalini hapo nimefanikiwa kuzungumza na Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Professa Mohamed Janabi, ambapo alibainisha maendeleo ya Mwambeta hospitalini hapo,kuendelea vyema kupata matibabu lakinmi akitanabaisha kwamba anahitaji matibabu ya hali na mali na msaada mkubwa hususani miguu ya bandia ambayo mguu moja unauzwa milioni 20.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube