BREAKING

Thursday 25 February 2016

RAIS WA MAGUFULI ATEMBELEWA NA UGENI KUTOKA GUINEA BISSAU..







JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Description: Description: Description: Description: Description: Coat of ArmsKURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz

Faksi: 255-22-2113425



OFISI YA RAIS,
      IKULU,
 1 BARABARA YA BARACK OBAMA,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais waJamhuri ya Guinea Bissau Mheshimiwa Jose' Mario Vaz amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa nchi hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali, hususani katika uchumi kwa manufaa ya wananchi wa nchi zote mbili.
Rais Jose' Mario Vaz amesema hayo katika ujumbe wa barua uliwasilishwa kwa Rais Magufuli na Mjumbe maalum wa Rais huyo Jenerali Omar Embalo, Ikulu Jijini Dar es salaam leo tarehe 25 Februari, 2016.
"Napenda kusisitiza kuwa nchi zetu ni marafiki wa muda mrefu, naomba urafiki na mahusiano haya mazuri yaendelee na ninakuhakikishia kuwa nchi yangu itaendelea kuuenzi ushirikiano huu" Ilieleza sehemu ya ujumbe huo.
Aidha, Rais Jose Mario Vaz amempongeza Rais Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano na amemualika kuitembelea nchi ya Guinea Bissau ili kuimarisha zaidi Uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Kwa upande wake Rais Magufuli amemshukuru Rais Jose Mario Vaz kwa kumtuma mjumbe maalum kwa ajili ya kumletea ujumbe wa pongezi, na amemhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Guinea Bissau.
"Nakushukuru sana Jenerali Umaro Sissoco Embalo kwa kuniletea ujumbe wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Guinea Bissau na nakuomba umwambie namshukuru kwa pongezi, mimi na serikali yangu tupo tayari kuimarisha uhusiano na ushirikiano na Guinea Bissau ili mataifa yetu yaweze kunufaika zaidi"Alisema Rais Magufuli
Wakati huo huo, Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Ikulu Jijini Dar es salaam leo.
Gerson Msigwa,
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
25 Februari, 2016

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube