BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Wednesday, April 09, 2025

Sunday, 13 August 2023

WANANCHI NGORONGORO WAOMBA KUHAMISHWA.



Baadhi ya Wananchi waliosalia ndani ya mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro (NCAA) wamewaambia Waandishi wa Habari kuwa wanaishi katika maisha ya tabu yasiyokuwa na huduma za kijamii na kwamba wanatamani kuondoka.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika kata za Nainokanoka na Naiyobi, wameeleza kuwa wanataka kuondoka kwa hiari kuwafuata wenzao katika makazi mapya ya Msomera huku wakiiomba serikali ya rais Samia ifanye hivyo haraka kwa kuwa hawaoni sababu ya kuendelea kuishi katika maeneo hayo.

Sinyati Emmanuel na Marry Kesumo Wanasema hawawezi kuishi mahali ambapo hakuna bara bara nzuri, maji,hospitali wala usafiri na kwamba hawana shughuli za maendeleo wanazozifanya kwa kuwa hawaruhusiwi hata kulima katika maeneo hayo.

Naye Jennifer Yuda kutoka kijiji cha Kapenjiro kata ya Naiyobi ambaye yupo tayari kuhama kwa hiari kutoka Ngorongoro kwenda Msomera, ameiomba serikali iwapatie maeneo kutokana na idadi ya Wake waliopo katika Boma husika.

Mosses Lenara ameishukuru Serikali kwa upendeleo ilioutoa kwao kwa kuwajengea nyumba Msomera na kuwapatia maeneo ya kilimo na ufugaji.

Serikali ilitoa nafasi ya kuwahudumia kila kitu ikiwa ni pamoja na kuwajengea Nyumba, Shamba na maeneo ya malisho, kuwasafirisha wao, mifugo na mizigo yao wote waliokubali kuhamia Msomera mkoani Tanga kwa hiari ili kupisha eneo hilo ambalo ni makazi ya wanyamapori wanaoingizia nchi mapato kupitia watalii.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube