BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Wednesday, 23 August 2023

PROF: HAMISI M. MALEBO AZUNGUMZIA UHAMISHAJI WANANCHI KATIKA HIFADHI YA NGORONGORO


’Uthibiti wa Magonjwa ya binadamu katika eneo la hifadhi ni changamoto kubwa, mbinu ambazo tunaweza kuzitumia nje ya hifadhi hatuwezi kuzitumia ndani ya hifadhi, kulingana na sheria za uhifadhi, katika eneo la ndani ya hifadhi hatuwezi kupulizia dawa ni mambo yasiyoruhusiwa, sasa Mwananchi anapokuwa pale analiletea pia Taifa changamoto kubwa ya namna ya kuendelea kumuhudia wakati yupo kwenye eneo ambalo lina vikwazo vingi katika masuala ya huduma za Afya na za Kijamii.

Wengine watashangaa kwamba kwa nini haya magonjwa tunayataja sana kwa Ngorogoro, maeneo mengine pia yapo lakini Ngorongoro ni eneo ambalo hawa wananchi wapo katika maeneo ambayo yamejitenga kuwafikia katika maeneo yao ni changamoto sana, kwa hiyo ule ugumu wa kuwapa huduma unawafanya waendelee kuteseka na magonjwa ambayo yanathibitika ni magonjwa ambayo tunaweza kuyakinga na kuyaondoa, tunaona Wananchi wanaishi katika hifadhi ya Ngorongoro lakini ukienda Mataifa mengine huwezi kukuta Wanadamu wanaishi katikati ya Wanyama pori.

Magonjwa yapo sehemu nyingine lakini kiwango cha Magonjwa katika hifadhi ya Ngorongoro ni kikubwa, ukiangalia changamoto anazozipata Mtoto mdogo wa chini ya miaka mitano aliyeko Ngorongoro ni kubwa kuliko Mtoto aliyeko Dar- es Salaam, Mwanza, Morogoro na sehemu nyingine, kwa mtu yeyote anayedhamini na kuheshimu ubinadamu kama angeweza kutembelea yale maboma na kuona maisha wanayoishi hawa watoto wadogo, hawana hata uhuru wa kucheza kwa sababu akisogea mita 5 tu anaweza kupitiwa na fisi, chui, Simba na wanyama wengine wakali yani hawa ni Watanzania wenzetu ambao wapo kwenye mazingira magumu na ya kutisha kwa mtu yeyote mwenye moyo wa huruma atafikiria tofauti’’.

Profesa Hamis ameseyasema hayo wakati alipokuwa katika  Mkutano wa mtandao wa Zoom, akizungumzia kuhusu awamu ya pili ya uhamishaji wananchi katika Hifadhi ya Ngorongoro

**HABARI HII KWA HISANI YA GILLY BONNY*****


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube