BREAKING

Wednesday 2 August 2023

KINANA -SHINA LA MUWA LINALOZALISHA VIKONYO KILA KUCHWAPO.







 MAKALA MAALUM-ZIARA YA KINANA

NA SAID MAKALA

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM  Abdulrhamani Kinana hivi karibuni aliihitimisha ziara yake ya ya siku 10 katika mikoa mitano,ziara ambayo ilikuwa mahususi katika utelezaji wa Ilani ya Chama hicho tawala cha CCM.

Katika Mikoa hiyo Kanali huyo mstaafu alizungumza mambo mengi kwa wanachi waiofurika katika mikutano yake ya hadhara lakini mengi  yakiwa yamejaa utamu wa chakula cha akili kama  mfano wa muwa uliojaa maji mengi na mtamu mithili ya asali , huku ukitafsirika kuwa na vikonyo kede kede shinani.

Katika ziara hiyo niliambatana naye niliona mengi ya kujifunza kutoka kwa Mwansiasa huyu nguli ambaye ama hakika ni wa kupigiwa mfano , katika ziara zake hizi si mara ya kwanza kuhuhudhuria huwa naburudika na maneno yake ya hekima yaliyojaa matumaini na hamasa ya kufufua fikra ambazo zilianza kufa kw awananchi ambao pengine katika maendeleo yao ya kiuchumi wanakutana na changamoto kadha wa kadha.

Akiwa Butiama Mkoani Mara nilimshuhudia kwa mara nyingine mzee Kinana akitoa tafsiri kubwa ya kuwaenzi mashujaa ambao wameipambania Tanzania katika kuleta ukombozi kutoka kwa Taifa jirani la Uganda, nakumbuka maneno haya aliyasema hivi

"Tuendelee  kuwaenzi mashujaa walioshiriki katika vita vya ukombozi dhidi ya nduli Idd Amin na shujaa wa kwanza ni Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye atabaki kuwa kielelezo wa Taifa la Tanzania"

Maneno hayo yalinikumbusha  maneno ya hekima na Buasara wakati Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini ambaye alichaguliwa kidemokrasia na Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ambaye alifariki Desemba 5, 2013 akiwa na umri wa miaka 95.

 Mandela anatambuliwa na taifa la Afika Kusini kwa kuleta mapinduzi ya Kiasisa kwani aliwahi kufungwa kwa kutumikia kifungo kwa miaka 27 kwa sababu ya mapambano yake dhidi ya mfumo wa kibaguzi wa Afrika Kusini unaofahamika kama  Ukaburu. Aliachiwa huru kutoka gerezani mwaka 1990, na kuwa rais miaka minne baadae, na kuachia madaraka baada ya kutumikia kwa kipindi kimoja tu, kitendo adimu kufanywa na wenye madaraka barani Afrika.

Akiwa mtu anayependwa duniani kote, Mandela alikuwa na namna ya mvuto katika maneno yake, Moja ya nukuu zake inatoka katika hotuba yake ya kijeuri aliyoitoa mahakamani wakati wa  kesi maarufu ya Uhaini ya Rivonia  mwaka 1964, ambapo. alisema "Nimepigana dhidi ya mfumo wa utawala unaowapendelea makaburu, na nimepigana dhidi ya mfumo wa utawala unaowapendela weusi. Nimekuwa na ndoto ya jamii ya kidemokrasia na huru ambayo watu wote wanaishi pamoja kwa mshikamano na fursa sawa. Ni ndoto ambayo nataraji kuiishi na kuitimiza. Lakini, kama itahitajika, hiyo ni ndoto ambayo nimejiandaa kupoteza maisha yangu kwa ajili yake."

Ukiacha hotuba hiyo ya kesi yake ya Rivonia, Mandela anaacha nyuma yake nukuu nyingi za kukumbukwa zenye busara alizozitoa katika kipindi chake chote cha uhai wake. Pamoja na kutuacha, anaendelea kuzungumza na ulimwengu kupitia watumiaji wa twita, ambao waliitikia habari za kifo chake kwa kusambaza maneno yake.

Maneno hayo ni ninayakumbuka sana kwa kuwa Mzee Kinana anendelea kutukumbusha na yeye ni mmoja wa watu wenye msimamo wa kusimamia maneno yenye Busara mtu ambaye hapendi kukwezwa, hata wasaidizi wake wanatambua hilo lakini mtu ambaye anatamani kuona mtanzania anapata haki ya kujenga historia bora ya kiuchumi.

Kinana, katika kauli zake akiwa Mkoani Mara kwenye mwendelezo wa ziara zake alitumia wasaa mwingi kutoa nasaha kwa watanzania kama alivyokumbusha watanzania kuthamini tarehe ya Julai 25 kuwaenzi Mashujaa .

Lakini katika hautua nyingine ambayo Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara Abdulrhaman Kinana katika ziara zake hizi akiwahutubia wanachi katika maeneo mbalimbali alifurahisha umma na wengine wakisema pembeni 'Huyu mzee jamani amebarikiwa kipawa cha kuongea" na maeneo hayo yalitoka pale alipowataka watanzania kuweka imani kwa Mhe. Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt .Samia Sukuhu Hassan  katika harakati zake za kuleta maendeleo nchini hususani kuwashawishi wawekezaji wakubwa kuja nchini kuwekeza.

Kauli hiyo akiibainisha katika Mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Mkendo Musoma mjini Mkoani Mara akitumia muda mfupi lakini wenye maneno yaliyojaa busara , ambapo pia hakuacha kuzungumzia masuala mazima ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM.

"  Kazi ya Serikali ni kutengeneza mazingira mazuri na kutoa  furusa ya kujiajiri kwa wananchi wake na kufanya kazi zao bila usumbufu wowote kwa kuwa huru zaidi wasikutane na changamoto katika kazi zao,ndio maana tupo katika ziara kuangalia CCM, imefanya nini,tupeni imani sisi CCM, kazi yetu ni kuleta maendeleo na si vinginevyo"Alisema Kinana...

MAKALA HII ITAENDELEA.....KUANGAZIA ZIARA YA MZEE KINANA...NA MAFAKIO YAKE.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube