BREAKING

Friday 25 August 2023

TANESCO YAONGEZA WATAALAM 20 MRADI WA BWAWA LA JNHPP



Muonekano wa Bwawa la Julius Nyerere






Mkurugenzi wa Tanesco Maharage Chande akizungumza katika mradi wa Bwawa la kufua Umeme wa Julius Nyerere









 Shirika la Umeme Tanzania TANESCO limesema tayari hatua ya kwanza ya wafanyakazi 20 kati ya wafanyakazi zaidi ya 200 wanaotarajiwa kuwasili katika mradi wa  uzalishaji Umeme waJulius Nyerere wamefika katika mradi huo.

Mkurugenzi wa TANESCO ,amesema hayo baada ya kuongoza jopo la menejimenti ya shirika hilo kujionea maendeleo ya mradi huo wa uzalishaji Umeme,ambapo amesema kwamba wafanyakazi hao ni wa kada mbalimbali ambao watakuwa wakifanya majukumu yao ndani ya mradi huo.

Akizungumzia taarifa ya Mamlaka ya hali ya hewa TMA juu ya uwepo wa mvua kubwa za Vuli ,amesema kuwa kama zitakuwepo  uwezekano wa bwawa hilo kujaa ni mkubwa ,huku akisema iwapo hazitakuwa na athari.

Katika hatua nyingine Chande akazungumzia maendeleo ya mradi kwa ujumla na kasi yake ,kama anavyobainisha huku baadhi ya watumishi wa Shirika hilo nao wakizungumzia maendeleo ya mradi huo

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube