BREAKING

Thursday 22 June 2017

MULTICHOICE TANZANIA YASAIDIA WATOTO YATIMA TANDALE

 Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania Baraka Shelukindo akikabidhi mashuka kwa Mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Madinnah kilichopo Tandale jijini Dar es Salaam Kuruthum Juma (wa pili kulia). Wa pili Kushoto ni Malkia wa Taarabu Hadija Kopa na kulia ni  Muigizaji maarufu wa tamthilia ya Huba Riyama Ali ambao ni mabalozi maalum wa DStv. 

 Watoto wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Almadinnah kilichopo Tandale wakipokea vyombo kutoka kwa Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania Baraka Shelukindo baada ya kupokea msaada wa vyakula na vifaa mbalimbali kutoka kampuni hiyo jana.

Mshonaji katika mradi wa ushonaji wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Al-Madinnah cha Tandale jijini Dar es Salaam Aziza Amri (wa pili kulia) akitoa maelezo kuhusu mradi huo unaofadhiliwa na kampuni ya Multichoice Tanzania. Kutoka kushoto ni Malkia wa mipasho Hadija Kopa ambaye ni balozi maalum wa DStv, Bi Kuruthum Juma ambaye ni mkuu wa kituo hicho, Baraka Shelukindo Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania na kulia ni Muigizaji maarufu wa tamthilia ya Huba Riyama Ali.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube