BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Thursday, 11 August 2016

WENGER AJITABIRIA ARSENAL,....

eneja wa klabu ya Arsenal ya Uingereza, Arsene Wenger amedai kwamba hatma yake katika klabu hiyo ya Emirates inategemea jinsi matokeo ya klabu hiyo msimu huu wa Ligi utakavyokuwa.

Amesema Mkataba wake utakamilika Juni mwakani kwa hivyo anategemea matokeo  ya msimu huu akiamini endapo atafanya vizuri huenda akaongezewa kandarasi nyingine ndani ya klabu hiyo.

Raia huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 66, aliajiriwa mwezi Septemba 1996 kuiongoza klabu hiyo, na kuipa mafanikio kadhaa lakini Mkataba wake wa sasa utakamilika mwishoni mwa mwezi juni mwaka ujao.

Arsenal haijashinda taji la ligi kuu ya Uingereza tangu mwaka wa 2004 jambo ambalo limechochea uhasama dhidi ya Wenger haswa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo.

Awali wenger alikuwa amehusishwa na wadhifa wa kocha wa timu ya Uingereza lakini Sam Allardyce akachaguliwa kuchukua nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube