BREAKING

Monday 1 August 2016

RAIS MAGUFULI AITULIZA NZEGA, ATAJA KERO ZA MAJI ZINATATULIKA HARAKA



0D6A3969

  • Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, Mh. Husein Bashe akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla. (kushoto). Wabunge hao walikuwa ndiyo wenyeji katika ugeni huo mkubwa kutokana na Rais kufanya mkutano ndani ya majimbo yao hayo.
0D6A3989
Rais Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla wakati Mh. Rais Magufuli alipowasili katika makazi ya Rais mjini Nzega akitokea Mkoa wa Singida alipoanzia ziara yake hiyo.

Bishop Chakupewa wa Nzega akitoa neno la Mungu wakati wa Mkutano huo wa Rais Magufuli alipotembelea Nzega, Mkoani Tabora. katika mkutano wa kushukuru Julai 30.
DSC_3660
Askofu Mzoka kutoka kanisa la Romani Cathoriki Nzega

DSC_3589
Mbunge wa Nzega Mjini, Mh. Hussein Bashe akitoa neno kwa wananchi wakati wa mkutano huo


DSC_3672
Mke wa Rais, Mama Janet Magufuli akisalimia wanannchi.
DSC_3712
Wananchi waliofurika wakishangilia wakati Rais Magufuli akipanda jukwaani
DSC_3682
Rais Magufuli akihutubia jukwaani.
DSC_3593
Sehemu ya umati wa tukio hilo..
DSC_3561
Rais Magufuli akitoa salamu kwa wananchi wa Nzega wakati wa kuelekea kupanda jukwaani. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli apongeza na kufurahishwa na juhudi za Wabunge Vijana wanaoongoza Majimbo ya Nzega Mjini ambalo linaongozwa na Mbunge Husein Bashe na lile la Nzega Vijijini linaloongozwa na Mbunge ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla. ambapo amewahakikishia kutatua kero zao kubwa ya maji ambayo inawakabili wananchi wengi katika Majimbo hayo.
Rais Dk. Magufuli ambaye aliweza kufanya mkutano mkubwa wa wazi ndani ya viwanja vya Nzega mjini, Julai 30, alibainisha kuwa, anafahamu matatizo wanayokabiliana nayo Wananchi wa majimbo hayo likiwemo suala hilo la maji ambapo amewaambia wamwachie alifanye kazi hilo huku suala lao la kutaka Mkoa mpya lisubiri kwanza mpaka atakapomaliza kero muhimu kwa wananchi ikiwemo kuwapatia huduma bora za afya, Madawa .
“Tatizo la Maji katika Wilaya Nzega ninalipokea na nitalifanyia kazi. Tanzania imepata mkopo wa dola za kimarekani Milioni 268.35 kutoka nchini India. Fedha ambazo zitatumika kutekeleza mradi wa kusambaza maji ya ziwa Viktoria katika Miji ya Tabora, Igunga, Nzega, Sikonge na Uyui pamoja na vijiji vilivyopo kandokando mwa bomba kuu kuanzia mwaka huu ambapo watu milioni moja na laki moja (1,100,000)watanufaika.” Alieleza Rais Magufuli.
Rais Magufuli ameongeza kuwa, Serikali imefanya usanifu na upembuzi yakinifu kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza maji ya kutoka mto Malagarasi kwa ajili ya Miji ya Urambo, Kaliua na Nguruka pamoja na vijiji vilivyopo kandokando mwa bomba kuu ambako watu laki sita (600,000) watanufaika hivyo katika tatizo la maji wananchi wa maeneo hayo wataondolewa kero yao kubwa ya maji.
Aidha, Rais Magufuli amepiga marufuku wakulima wadogo kutozwa ushuru wa mazao watokapo na mazao mashambani.
"Ninapenda tukusanye kodi, lakini sio kukusanya kodi kutoka kwa watu masikini, mtu ametoka shambani na magunia yake mawili au hata matano halafu nyinyi mnamtoza kodi.
"Mimi sipendi kuwanyanyasa hawa watu wanyonge, mtu akiwa na mazao lori zima hapo sawa lakini sio kwa mtu mnyonge mwenye gunia moja" Amesema Rais Magufuli wakati wa kutoa taarifa maalum ya kuzuia watu wanaonyanyasa wakulima wadogowadogo pamoja na wananchi katika suala la kuwakusanyia ushuru.



No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube