BREAKING

Monday 1 August 2016

MO ASEMA AVEVA ASIOGOPE UKUBWA.





Baada ya Uongozi wa klabu ya soka ya Simba na wanachama wake kufanya mkutano wao mkuu jana na kujadili mambo mbalimbali huku ajenda kubwa ikiwa ni kujadili juu ya klabu hiyo kuendeshwa kitaalamu kwa njia ya hisa hatimaye fanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji maarufu kwa jina la Mo ameibuka na kusema tayari ameandika barua kwa uongozi wa Simba kueleza kuhusiana na uamuzi wake wa kutaka kununua hisa za Simba kwa asilimia 51.

Mo amesema ameandika barua hiyo leo asubuhi baada ya kusikia baadhi ya viongozi wa Simba wakisema hakuwa amefanya hivyo,ambapo amesema alichokiandika ndani ya barua hiyo ni kuueleza uongozi huo kutoa ofa ya Sh bilioni 20 ili kupata hisa asilimia 51, huku akikanusha kauli za uongozi huo katika mktano wa jana kwamba hajawahi kukutana na viongozi hao ambapo amesema amewahi kukutana na Rais wa Simba, Evans Aveva zaidi ya mara tatu.

Mo amesema katika barua hiyo ameandika mambo mbali mbali ikiwepo kueleza kuwa ni mwanachama aliyewahi kuwa mfadhili wa timu, ambaye sasa anataka awekeze Sh. Bilioni 20 kwa kununua asilimia 51 ya hisa za klabu.

Baada ya kufanya mkutano huo na waandishi wa habari muda mfupi Mo alipokea barua kutoka Uongozi  wa Simba kujadiliana naye juu ya mpango wa kununua hisa za klabu hiyo.

Katika barua iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa klabu, Patrick Kahemele leo uongozi wa Simba umemuomba Mo Dewji kuhudhuria kikao cha Kamati ya Utendaji Agosti 15, mwaka huu.

Katika barua hiyo imeeleza kikao hicho kifanyike Agosti 15 kwa sababu wiki hii watakuwa wametingwa na shughuli za wiki ya Simba kuelekea tamasha la Simba Day Agosti 8, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube