BREAKING

Thursday 2 August 2018

ARSENAL YATOKA NYUMA NA KUIZIMA CHELSEA KWA MATUTA






Mshambuliaji Alexandre Lacazette akishangilia baada ya kuifugia Arsenal bao la kusawazisha dakika ya 90 na ushei ikitoa sare ya 1-1 na Chelsea katika mchezo wa kirafiki wa Kombe la Mabingwa wa Kimataifa Uwanja wa Aviva mjini Dublin kufuatia Antonio Rudiger kuanza kuifungia The Blues dakika ya tano. Arsenal ikaenda kushinda kwa penalti 6-5 kufuatia Ruben Loftus-Cheek kukosa penalti ya mwisho ya Chelsea na Alex Iwobi kufunga kwa upande wa Washika Bunduki wa London, ambao wapo chini ya kocha mpya, Mspaniola, Unai Emery aliyechukua nafaisi ya Mfaransa, Arsene Wenger mwezi uliopita. Waliofunga penalti za Arsenal ni Alexandre Lacazette, Reiss Nelson, Matteo Guendouzi, Ainsley Maitland-Niles, Mesut Ozil na Alex Iwobi wakati za Chelsea zimefungwa na Danny Drinkwater, Tammy Abraham, Victory Moses, Emerson na Lucas Piazon













No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube