BREAKING

Monday 14 August 2017

RONALDO ALIMVYOJIBU MESSI KWA KUWASOMESHA JEZI YAKE MASHABIKI WA BARCELONA PALE CAMP NOU




Kama unakumbuka ilikuwa Aprili, mwaka huh pale Lionel Messi aliposhangilia baada ya kufunga bao mwishoni katika El Clasico kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu, Madrid, akaamua kushangilia kwa kuwaonyesha mashabiki wa Madrid jezi yake.

Messi aliionyesha jezi hiyo kwa mashabiki wa Madrid na kuzua gumzo, lakini leo Cristiano Ronaldo naye amejibu akiwaonyesha mashabiki wa Barcelona jezi namba 7, waisombe baada ya kufunga bao la pili katika mechi ya Spanish Super Cup.

Madrid imeshinda kwa mabao 3-1 katika mechi hiyo lakini Ronaldo aliyeingia, alikumbana na red card baada ya kupata yellow mbili. Mechi ya pili dhidi ya timu hizo itakayopigwa Agosti 17 kwenye dimba la Santiago Bernabeu itaamua bingwa.

Baada ya kufunga bao hilo alivua jezi na kuwaonyesha mashabiki hao, sawasawa na alivyofanya Messi, Aprili, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube