BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Wednesday, 9 August 2017

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA BANDA LA COSTECH MAONYESHO YA NANENANE KITAIFA NGONGO MKOANI LINDI

 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan (kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, HusseinMansour (hayupo pichani), alipotembelea banda la Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), kwenye Maonyesho ya Nanenane viwanja vya Ngongo mkoani Lindi leo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu. Maonyesho hayo yatafungwa na Makamu wa Rais leo mchana.

Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, HusseinMansour (kushoto), akitoa maelezo kwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, alipotembelea banda la COSTECH.
Mtafiti kutoka COSTECH, Bestina Daniel, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda la COSTECH katika maonyesho hayo.
Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni (MARI), Christina Kidulile, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda la COSTECH jinsi ya kuotesha mimea kwa kutumia chupa.
 Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia (OFAB), Philbert Nyinondi, kushoto akizungumza na wadau wa kilimo jinsi Maktaba ya Taifa ya Sokoine ya Kilimo-SNAL itakavyowawezesha wakulima wa Tanzania kupata taarifa za kilimo kwa njia rahisi.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), Patric Ngwediage (wa nne kulia), akiwa na Crew nzima ya COSTECH katika banda hilo.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia (OFAB), Philbert Nyinondi (katikati) akigawa vipeperushi kwa wakulima ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), vinavyohusu Maktaba ya Taifa ya Sokoine ya Kilimo-SNAL. Kushoto ni Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni (MARI), Christina Kidulile.


Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga Kilosa mkoani Morogoro, Ismail Ngolinda, akitoa maelekezo kwa wakulima jinsi ya kuotesha miche kwa njia ya chupa.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube