BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Wednesday, April 09, 2025

Thursday, 23 March 2017

NAPE AMSHUKURU RAIS KWA KUMUAMINI KWA MWAKA MMOJA, APONGEZA PIA UTEUZI WA MWAKYEMBE


 na2
Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amewataka Watanzania kukubaliana na suala la  kusitishwa kwake uteuzi wa cheo hicho.
Rais John Magufuli amemteua Dk Harrison Mwakyembe kuchukua nafasi hiyo ya Nape.
Akizungumza na waandishi nje yaHOTELI ya Protea, leo. Nape amesema wanatakiwa kukubaliana na hali halisi.
“Mkubali Tanzania ni kubwa kuliko Nape na hampaswi kuanzisha matatizo. Tanzania ni nchi yetu sisi na tujue Nape hawezi kuwa mkubwa kuliko Tanzania.
“Nawashauri kuwa watulivu, namshukuru Rais Magufuli kwa kunipa nafasi ya kufanya naye kazi kwa mwaka mzima.
“Nilifanya kazi yangu kwa akili na nguvu zangu zote. Nawashukuru wasanii, waandishi, wanamichezo kwa ushirikiano wenu. Nilipenda kuendelea kufanya kazi nanyi lakini muda wa aliyeniteua umefika, nitawakumbuka sana, ninawapenda sana,” alisema Nape.
Wakati anataka kuondoka katika eneo hilo, gari lake lilizuiwa na RPC wa Kinondoni, Suzan Kaganda hali iliyosababisha taharuki hadi Nape aliwapowaomba waandishi kuondoka eneo hilo ili naye aondoke.

na3
na1
Baadhi ya maaskari wakiwa wameimarisha ulinzi katika eneo hilo.
na4
Gari la Kamanda wa polisi mkoa wa Kindondoni likiwa katika eneo la tukio.
na5na6

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube