BREAKING

Thursday 2 March 2017

NAHODHA WA ZAMANI WA KLABU YA LIVERPOOL INAYOSHIRIKI LIGI KUU NCHINI UINGEREZA JOHN CHARLES BARNES ATUA NCHINI KWA AJILI YA KUENDESHA KLINIKI YA SOKA


Mshambuliaji wa zamani wa timu ya Liverpool, John Barnes,akiwasili 




Mshambuliaji wa zamani wa timu ya Liverpool, John Barnes na mchambuzi wa soka husani Ligi ya Uingereza ametua nchini tayari kwa ajili ya kuendesha kliniki ya soka kwa vijana wa timu ya taifa chini ya miaka 17 Srengeti Boy's.

Sambamba na hilo Barnes pia atahudhuria awamu ya pili ya mashindano maalumu ya kombe la Standard Chartered ambayo yatashirikisha timu tatu kutoka nchiza za Tanzania, Kenya na Uganda.

Mara baada ya kuwasili Barnes amezungumzia ujio wake na jinsi atakavyokutana na vijana wa Serengeti Boy's huku akisifia programu mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na wadau wa soka akibainisha kuwa japo ni mara yake ya kwanza kutua nchini lakini amekuwa akifuatialia maendeleo ya soka hususani Afrika Mashariki, huku akitambua uwepo wa nyota anayecheza soka la kulipwa Ubelgiji Mbwana Samatta, ambapo amesema ili timu zifanye vizuri lazima kuwekeza kwa vijana.

Kwa upande wake Afisa Habari wa Shirikisho la soka Tanzania TFF Alfredy Lucas pamoja na Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Standard Chartered Tanzania wamesema kuwa ujio wa Barnesw una faida nyingi ikiwepo kuwahamasisha vijana pamoja na kuimarisha vipaji vya soka kwa vijana wa Kitanzania 

Wamesema kuwa wanaamini kuwa Barnes atatumia ujuzi wake kadri atakavyoweza ili kuwanufaisha vijana wenye vipaji 

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube