BREAKING

Wednesday 15 March 2017

TENGA AOMBEWA DUA NJEMA NA BODI YA LIGI KUU TANZANIA BARA,UCHAGUZI MKUU WA CAF






Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kupitia Mkurugenzi wake, Boniface Wambura imewaomba wadau wa michezo nchini kumwombea dua ya ushindi, Rais wa Heshima wa Shirikisho la soka Tanzania TFF, Leodgar Tenga, ili aweze kushinda nafasi ya ujumbe katika Baraza la FIFA.

Akiwa katika mahojiano maalum na kituo hiki Wambura amesema kuwa itakuwa heshima kubwa iwapo Tenga atapata nafasi hiyo ya ujumbe, kutokana na uwezo wake katika kuendeleza soka.

Wambura amesema hayo huku kesho ikiwa ndio siku mhimu ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa CAF kuadhimisha miaka 60,ya kuzaliwa kwa CAF pamoja uchaguzi wa kumpata rais mpya wa Shirikisho la soka Afrika CAF

Sambamba na hilo Wambura pia ameitakia kila la kheri Zanzibar kupata uanachama wa CAF na FIFA.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube