BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Thursday, April 10, 2025

Wednesday, 27 January 2016

SERIKALI YATOA AGIZO LA MASHIRIKISHO YA MICHEZO KUFUATA TARATIBU ZA MICHEZO ILI KUEPUKA MIGOGORO

nape-FILEminimizer

 
Serikali imetoa wito kwa Vyama,Vilabu na Mashirikisho ya mpira wa miguu kuzingatia na kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa katiba zao ili kupunguza migogoro inayoweza kujitokeza katika uendeshaji na uendelezaji wa soka nchini.
Hayo yamesemwa Leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura  wakati akijibu swali la Mhe. Khatibu Saidi Haji Mbunge wa Konde (CUF) kuhusu makosa yanayofanywa na  klabu za soka nchini kwa kupeleka mambo ya kisoka katika mahakama  ambapo ni kinyume cha sheria za FIFA.
Mhe. Annastazia Wambura amesema ni kweli kuwa Sheria za FIFA zinakataa mambo yanayohusiana na soka kupekekwa mahakamani hivyo hatua hiyo ya Vyama na Klabu kuzingatia Sheria na taratibu inalenga kuwezesha masuala ya soka kuendeshwa kwa  kuzingatia taratibu na miongozo iliyowekwa na Mamlaka za Michezo huo kwa ngazi mbalimbali.
Aidha amesema hatua hiyo imewezesha mchezo wa soka kuchezwa na kupata  matokeo kwa wakati na hivyo kuepusha mazuio ya mahakama ambayo yanaweza kusababisha usumbufu usio wa lazima kwa washiriki wengine hata kupelekea kufungiwa kwa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF).
Maendeleo ya michezo hapa nchini yanaendeshwa kwa mujibu wa Sheria ya Baraza la Michezo ya mwaka 1967, kama ilivyorekebishwa kwa mujibu wa Sheria Na 6 ya mwaka 1971 lakini bado  Sheria hii inakinzana na Sheria za FIFA ila serikali inafanya mapitio ya Sheria hiyo ili iendane na wakati kwa lengo la kuboresha na kuendeleza michezo nchini.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube