BREAKING

Tuesday 5 January 2016

REAL MADRID ILIVYO MUONYESHA NJIA YA KUTOKEA BENITEZ......

  Rafael Benitez Out Madrid

 Zinedine Zidane in Madrid

Mwanandinga wa zamani wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa  Zinedine Zidane ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu ya Real Madrid akirithi mikoba ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mhispania Rafael Benitez.

Zidane almaarufu kama Zizou amechukua nafasi hiyo ikiwa ni miezi saba tangu Rafael Benitez akamatie kiti hicho na kuifanya klabu hiyo  kuwa na mwenendo mbaya ikiwemo sare ya bao 2-2 na Vallencia na kupelekeaMabingwa hao wa zamani wa la liga kushika nafasi ya 3 wakiachwa alama 4 na kinara wa ligi ya hispania klabu ya Athletico Madrid.

Zidane mwenye miaka 43 ambae alishinda mataji akiwa na Real Madrid katika ngazi ya uchezaji alitangazwa  mapema jana na Mmiliki wa klabu hiyo Florentino Perez's akittokea kukinoa kikosi B cha real Madrid.

Mfaransa huyo atakuwa kocha wa 11 katika kipindi cha miaka 12 kupata kukinoa kikosi hicho wakati kibarua chake cha kwanza kikiwa dhidi ya Deportivo la Coruna siku ya Juamosi.


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube