BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Monday, 4 January 2016

ZOEZI LA KUWEKA ALAMA ZA X KWENYE NYUMBA ZINAZOPASWA KUBOMOLEWA LIMMEENDELEA KATIKA MAENEO YA MABONDENI JIJINI DAR ES SALAAM CHINI YA ULINZI MKALI WA JESHI LA POLISI KIKOSI CHA KUTULIZA GHASIA


Zoezi la kuweka Alama za X kwenye nyumba zinazopaswa kubomolewa limeendelea leo katika maeneo ya mabondeni jijini Dar es Salaam ambapo nyumba zaidi ya 3500 zimewekwa alama hiyo katika eneo la bonde la mto Msimbazi.

**Katika kutekeleza zoezi hilo, zaidi ya askari elfu moja wa kikosi cha kuzuia ghasia FFU cha Jeshi la Polisi wameimarisha Ulinzi katika maeneo mbalimbali ya mabondeni kutokana na kushambuliwa kwa mawe hivi karibuni baadhi ya maafisa kutoka ardhi waliokuwa wakiendesha zoezi hilo katika maeneo ya jangwani ambapo wananchi pia walifunga barabara kwa matairi na kuchoma moto kupinga zoezi hilo.

Maeneo yaliyokumbwa na zoezi la kuwekwa alama za x ni pamoja na nyumba zote zilizopo eneo la jangwani, upande wa kigogo sambusa,kigogo mbuyuni pamoja na nyumba zilizopo katika eneo la sukita , ambapo utekelezaji wa kuweka alama hizo umewaacha baadhi ya wamiliki wakiangua vilio ,wengine kuanguka na kupoteza fahamu huku baadhi wakiduwaa kwa kushindwa kujua hatua gani wachukue kutokana na wengine kuwa na majengo mapya ya gharama ambayo wamejenga kando ya mto msimbazi.

Akizungumza na mtandao huu wa Shamakala360 Afisa mwandamizi kutoa baraza la taifa la usimamizi wa mazingira NEMC- Anold Kisiraga amesema zoezi la kubomoa nyumba linaanza rasmi kesho kwa wale waliopinga kubomoa kwa hiari yao huku pia akisisitiza kuwa zoezi hilo litaenda sambamba na uwekwaji wa alama za x kwenye nyumba ambazo zitakumbwa na zoezi hilo.

Wakati huo huo Ombi la wakazi zaidi ya 600 wa mabondeni wakiongozwa na Mbunge wa Kinondoni ambao wamefungua kesi katika mahakama ya kuu kitengo cha ardhi kusitishwa zoezi hilo limesogezwa mbele mpaka kesho saa tano .

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube