BREAKING

Wednesday 3 January 2024

SERIKALI YANUFAIKA NA ZAIDI YA BILIONI 600.…




Serikali imesaini mikataba mitano ya uwekezaji Mahiri kwa wawekezaji wa wanyama pori nchini ambapo Serikali itanufaika na zaidi ya shilingi bilioni mia sita tisini za kitanzania  ikiwa na lengo la kuvutia na kuendeleza vivutio vilivyopo nchini vinavyomilikiwa na  mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania (TAWA) ikiwa ni jitihada za rais wa awamu ya sita Mh Rais Dkt Samia Suluu Hassan katika kukuza utalii wa ndani  na kuwanufaisha watanzania wote.....

Waziri wa maliasili na utalii Angela Kairuki amesema hii ni nafasi kwa serikali ya Tanzania kupitia Mhe Rais  samia kuboresha mazingira rafiki ya uwekezaji na kuendelea kuwavutia wawezekaji na kuongeza idadi ya wawekezaji nchini

Kwa upande wake Mkurugenzi wa bodi ya wakurugenzi ya (TAWA) Hamis Semfuko amesema lazima kuboresha miundombinu ambayo inamilikiwa na tawa ili kuvutia utalii wa ndani katika maeneo mbali mbali…

Mmoja kati ya wawekezaji katika hafla hiyo Taral Abood amesema kupitia uwekezaji huo wanaenda kutekeleza na kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya sita katika kupiga hatua za kimaendeleo…

Hafla hiyo ya utiaji wa saini ya mikataba sita umehudhuriwa na wakala wa misitu tanzania tfs, mamlaka ya usimamizi wa nyamapori tanzania tawa, na wawekezaji pamoja na wadau kutoka sehemu mbali mbali.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube