BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Wednesday, April 09, 2025

Friday, 5 January 2024

MAGIFTI DABODABO YA TIGO -MUUZA MATUNDA ALAMBA MIL.5...



Kampeni ya Magifti Dabodabo inayoendeshwa na Kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Tigo, imewakabidhi mamilioni yao washindi wa kampeni hiyo waliopatikana wikiendi iliyopita.

Katika tukio hilo washindi watatu, Flazia Issa, Stephano Mgova, Shabani Juma walikabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja na Kiungi Juma alikabidhiwa shilingi milioni tano alizojishindia.

Akiwakabidhi mfano wa hundi ya fedha walizojishindia Semaji la Kampeni hiyo, Haji Manara aliwapongeza washindi hao na kuwataka wakawe mabalozi wazuri wa kampeni kwani wao ndiyo mashuhuda wakubwa wa ukweli na uwazi wa kampeni hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Bidhaa za Tigo, Ndevorael Eliakimu aliwataka watumiaji wa simu za mkononi kutumia mtandao wa Tigo kwa huduma mbalimbali kama vile kufanya miamala, kulipa bili na malipo mengine, kununua vocha kwa kutumia Tigo Pesa au za kukwangua na huduma nyinginezo.

Eliakimu amesema kampeni bado inaendelea ambapo pamoja na pesa taslimu kuna zawadi za seti ya vifaa vya nyumbani vya kisasa kutoka Kampuni ya Hisense ikiwemo friji, runinga, microwave na seti ya muziki (sound bar).

Sambamba na zawadi hizo, Eliakimu amesema kuna zawadi kubwa za magari mapya kabisa ya kisasa ambapo zawadi zote hizo zitatolewa mara mbili kwa kila mshindi na mpendwa wake kama inavyoitwa kampeni hiyo Magifti Dabo dabo.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube