BREAKING

Wednesday 31 January 2024

WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUTOKA MATAIFA 8 KUSHIRIKI TAMASHA LA PASAKA 2024



Kuelekea Tamasha la Pasaka mwaka 2024 Alex Msama Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion waandaaji wa Tamasha hilo amethibitisha waimbaji wa muziki wa injili kutoka mataifa  zaidi ya 8 watakuwepo kwenye Tamasha la Pasaka la mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Alex Msama kuwa maandalizi makubwa kuelekea Tamasha hilo yamekwisha fanyika kwa asilimia kubwa na watu wakae mkao wa kula kwani Tamasha la mwaka huu litakuwa na zuri na lenye shangwe kubwa sana kwa wakazi wa mkoa wa Dar es salaam.

Tamasha la mwaka huu litafanyika siku ya Jumapili ya Pasaka, huku kauli mbiu ikiwa ni ASANTE MUNGU KWA KUTUPA RAIS SAMIA S HASSAN MCHAPA KAZI



Thursday 25 January 2024

TAMASHA LA PASAKA 2024 KUANZIA JIJINI DAR ES SALAAM,MACHI 31


Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion Alex Msama ametangaza Tamasha la Pasaka mwaka 2024  linatarajia kuanza kufanyika katika mkoa wa Dar es Salaam siku ya Pasaka tarehe 31 mwezi 3 mwaka 2024

Waimbaji mbali mbali wa muziki wa Injili watashiriki katika  Tamasha hili kubwa la Pasaka kwa mwaka 2024.

Maandalizi makubwa yanaendelea kufanyika, na Tamasha la mwaka huu limekuja na kauli mbiu inayosema "

 ASANTE MUNGU KWA KUTUPA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN MCHAPA KAZI.....

Monday 22 January 2024

SPORTPESA WAIUNGA MKONO TAIFA STARS AFCON KWA PROMOSHEN


 Afisa wa Idara ya Uhusiano na Mawasiliano SportPesa Lydia Solomon, akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya Sportpesa AFCON

RAIS SAMIA :JESHI LA WANANCHI JWTZ JIPANGENI UCHAGUZI UNAKUJA




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Lugalo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufungua Mkutano wa CDF na Makamanda kwa mwaka 2023 tarehe 22 Januari, 2024.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania (CDF) Jenerali Jacob John Mkunda kabla ya kufungua mkutano wa Makamanda kwa mwaka 2023 uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.




Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Maafisa Majenerali mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wakiimba Wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kwa mkutano wa CDF na Makamanda uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.


Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Maafisa Majenerali mbalimbali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wakiwa kwenye Mkutano wa CDF na Makamanda uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala kwenye picha ya pamoja na Maafisa Wanawake wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kufungua Mkutano wa CDF na Makamanda kwa mwaka 2023 uliofanyika Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Januari, 2024.

Monday 15 January 2024

KATIBU MKUU MPYA CCM USO KWA USO NA RAIS SAMIA


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Emmanuel John Nchimbi mara baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo kwenye Kikao Maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kilichokutana tarehe 15 Januari, 2024 Mjini Unguja Zanzibar.chimbi



 

EMMANUEL NCHIMBI KATIBU MKUU CCM..



Emmanuel Nchimbi ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama cha Mapinduzi (CCM).Akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Daniel Chongolo ambaye alijiuzulu.


KAMISHNA MABULA AFANYA UKAGUZI WA KARAKANA YA KISASA MANYONI, ATOA MAELEKEZO MAHSUSI









Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda ameeleza kufurahishwa kwake na ubora wa viwango vya ujenzi wa karakana ya matengenezo ya magari na mitambo iliyojengwa Kanda ya Kati ya TAWA wilayani Manyoni, karakana inayotajwa kuwa ni kubwa kuliko karakana zote zilizojengwa na taasisi hiyo.

Ameyasema hayo  Januari 14, 2024 akiwa katika ziara yake Makao Makuu ya Kanda ya Kati ya TAWA wilayani Manyoni, ziara yenye lengo la kukagua shughuli za uhifadhi na utalii zinazotekelezwa na TAWA wilayani humo.

"Nimetembelea na kukagua karakana, kimsingi nimeona imejengwa vizuri na pia nimeona ina uwekezaji mkubwa wa vifaa vitavyotumika na nina imani hii karakana itatusaidia sana" amesema

Akibainisha sababu za kuifanya karakana hiyo kuwa kubwa wilayani humo, Kamishna Mabula amesema Manyoni ni katikati ya nchi na ni sehemu inayofikika kwa urahisi, hivyo kutokana na ukubwa wake itatumika kutengeneza magari si tu ya Kanda ya Kati bali ya taasisi nzima.

Aidha, Kamishna Mabula ameuelekeza uongozi wa Kanda hiyo kuweka mfumo madhubuti wa usimamizi wa karakana ikiwa ni pamoja na kuwapeleka wataalamu wa vifaa hivyo ili iweze kusimamiwa na kuendeshwa Kisasa.

Vilevile Kamishna Mabula ametumia ziara hiyo kuwahimiza Maafisa na Askari wote wa TAWA kurejea mpango mkakati wa  taasisi hiyo ambao unafikia kikomo Mwaka 2026 ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Amefafanua kuwa mpango mkakati wa TAWA una malengo makuu matatu ambayo ni kuhakikisha rasilimali ambayo TAWA imepewa kusimamia inakuwa salama, pia kuhakikisha wateja wote wa taasisi wakiwemo wawekezaji wanapata huduma na kuridhika na huduma inayotolewa na lengo la tatu ni kuhakikisha TAWA inafanya kazi kwa ufanisi na tija.

Kamishna huyo amesisitiza kuwa malengo hayo hayataweza kutimia bila kuishi  katika tunu za taasisi hiyo ambazo ni uadilifu, kufanya kazi kwa ushirikiano, kutenda kazi kwa ubunifu pamoja na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.

Naye Kamishna Msaidizi Ulinzi wa Rasilimali za Wanyamapori Hadija Malongo akimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa Kanda ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia TAWA kwa kuwezesha ujenzi  wa karakana hiyo ambayo kukamilika kwake kutasaidia kupunguza gharama za matengenezo ya magari ambayo ilikuwa changamoto kubwa

Mradi wa ujenzi wa karakana hiyo umegharimu zaidi ya TZS Million 217.

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO MAALUM CHA KAMATI KUU CCM






Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao Maalum cha Kamati Kuu  ya Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika Leo tarehe Januari  15, 2023 Unguja, Zanzibar

Thursday 11 January 2024

MKAZI WA KAGERA OLIVIA PASTORI AKABIDHIWA MIL. 10 ZA MAJIFTI DABODABO KUTOKA TIGO


Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Joseph Mutalemwa(kulia) akimkabidhi mfano wa hundi Shilingi milioni kumi Mshindi wa Magifti Dabodabo mkazi wa kijiji cha Rushaka, Kitongoji cha Bweigilo kata ya Bwendangabo wilayani Bukoba mkoani Kagera Olivia Pastory baada ya kuibuka mshindi katika hafla iliyofanyika nyumbani kwao mshindi,katikati ni Meneja wa Tigo Mkoa wa Kagera Robert Paul akishuhudia.

Tuesday 9 January 2024

MLOGANZILA WAZINDUA HUDUMA YA MAFUNZO YA WAGONJWA WA KIHARUSI








Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa kushirikiana na Taasisi ya Kiharusi Duniani (The World Stroke Organization) imezindua mafunzo maalumu kwa wataalamu wanaoshughulikia magonjwa ya kiharusi kwa lengo la kuendelea kuboresha huduma kwa wagonjwa hao.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya nje (OPD) Dkt. Elimeena Meda amesema mafunzo hayo ni muhimu kwani kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa kiharusi hivyo ni muhimu watoa huduma wote kujua namna bora ya kuwahudumia wagonjwa hao.

“Tumeona sababu ya kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa kiharusi, mafanzo haya yanahusu kada zote zinazoshiriki katika mnyororo wa kuwahudumia wagonjwa wa kiharusi ili kuboresha huduma wanapokuwa hospitalini hadi wanaporuhusiwa” ameongeza Dkt. Meda.

Kwa upande wake, muandaaji wa mafunzo hayo kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Sarah Matuja amebainisha kwamba ugonjwa wa kiharusi umekuwa tishio nchini na unawakumba watu wenye umri wa miaka kati ya miaka 40 hadi 60 na hivyo kuathiri nguvu kazi ya jamii.

Mafunzo hayo yanatolewa na wataalamu bingwa wa magonjwa ya kiharusi duniani kuanzia leo Januari 9 hadi Machi 19, 2024 ambapo yatahusisha wakufunzi ambao ni Madaktari Bingwa wa kiharusi duniani na yatafanyika kwa nadharia na vitendo.

TIGO WADHAMINI WA MAONYESHO YA KIBIASHARA ZANZIBAR


Mkurugenzi wa kanda Tigo Zantel, Aziz  Said Ali, akimuelezea Mshafanyabiashara wa Mwani,  Jaha Haji Khamis kuhusu huduma ya Mjasiriamali box katika maonesho ya kibiashara Zanzibar,ambapo Tigo zantel ni mdhamini mkuu wa maonesho hayo.

Saturday 6 January 2024

DKT. BITEKO- TUYAENZI NA KUYALINDA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR



Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kuyaenzi, kuyalinda na kuyaishi kwa dhamira ya dhati, Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwani Waasisi wa Nchi  walifanya mapinduzi hayo ili kuwa na Taifa huru ambalo kila mtu anakuwa na hadhi, kuondoa dhuluma iliyokuwepo na kufanya wananchi kuishi kwa amani na furaha.

Amesema hayo tarehe 6 Januari 2024 wakati akizungumza na Wananchi  katika Wilaya ya Mkoani, mkoani Kusini Pemba mara baada ya kuzindua Afisi ya Uhamiaji na Makaazi ya Askari wilayani humo.

“Sisi Wananchi tunawajibu wa kuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kuyaishi, kuyaheshimu,  kukuza uchumi wa nchi na kukuza uzalendo ili baada ya muda mrefu hata baada ya miaka 100 mbele, watakaokuja kusherehekea Mapinduzi haya wakute Zanzibar iliyobora zaidi na waseme Mapinduzi haya yalitufaa.” Amesema Dkt. Biteko

Ameeleza kuwa, moja ya tunu tuliyonayo ni mshikamano hivyo watu wasiruhusu mtu yoyote kuwagawanya kwa misingi yoyote ile, bali maendeleo yaunganishe watu wote na kwamba tofauti za vyama, dini na  kabila visifanye watu wakae kwenye makundi bali kuunganisha watu kwa maslahi ya nchi na watanzania.

Amesema kuwa, nchi inapoenda kusherehekea Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar tarehe 12 Januari mwaka huu, watanzania wote waungane kuwaombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi, ili waendelee kuongoza vyema, kuimarisha ustawi wa Taifa na kuwaunganisha Watanzania.

Kuhusu Jengo hilo jipya la Afisi ya Uhamiaji katika Wilaya ya Mkoani, mkoani Kusini Pemba, Dkt, Biteko amesema kuwa ni moja ya matunda ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 kwani kabla ya Mapinduzi watu walinyimwa haki zao za kimsingi zikiwemo za uhamiaji kama vile kupata pasi ya kusafiria na hivyo Mapinduzi yamewezesha wananchi kupata uhuru wa kusafiri nje ya mipaka ya nchi.


Friday 5 January 2024

MAGIFTI DABODABO YA TIGO -MUUZA MATUNDA ALAMBA MIL.5...



Kampeni ya Magifti Dabodabo inayoendeshwa na Kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Tigo, imewakabidhi mamilioni yao washindi wa kampeni hiyo waliopatikana wikiendi iliyopita.

Katika tukio hilo washindi watatu, Flazia Issa, Stephano Mgova, Shabani Juma walikabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja na Kiungi Juma alikabidhiwa shilingi milioni tano alizojishindia.

Akiwakabidhi mfano wa hundi ya fedha walizojishindia Semaji la Kampeni hiyo, Haji Manara aliwapongeza washindi hao na kuwataka wakawe mabalozi wazuri wa kampeni kwani wao ndiyo mashuhuda wakubwa wa ukweli na uwazi wa kampeni hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Bidhaa za Tigo, Ndevorael Eliakimu aliwataka watumiaji wa simu za mkononi kutumia mtandao wa Tigo kwa huduma mbalimbali kama vile kufanya miamala, kulipa bili na malipo mengine, kununua vocha kwa kutumia Tigo Pesa au za kukwangua na huduma nyinginezo.

Eliakimu amesema kampeni bado inaendelea ambapo pamoja na pesa taslimu kuna zawadi za seti ya vifaa vya nyumbani vya kisasa kutoka Kampuni ya Hisense ikiwemo friji, runinga, microwave na seti ya muziki (sound bar).

Sambamba na zawadi hizo, Eliakimu amesema kuna zawadi kubwa za magari mapya kabisa ya kisasa ambapo zawadi zote hizo zitatolewa mara mbili kwa kila mshindi na mpendwa wake kama inavyoitwa kampeni hiyo Magifti Dabo dabo.

Wednesday 3 January 2024

SERIKALI YANUFAIKA NA ZAIDI YA BILIONI 600.…




Serikali imesaini mikataba mitano ya uwekezaji Mahiri kwa wawekezaji wa wanyama pori nchini ambapo Serikali itanufaika na zaidi ya shilingi bilioni mia sita tisini za kitanzania  ikiwa na lengo la kuvutia na kuendeleza vivutio vilivyopo nchini vinavyomilikiwa na  mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania (TAWA) ikiwa ni jitihada za rais wa awamu ya sita Mh Rais Dkt Samia Suluu Hassan katika kukuza utalii wa ndani  na kuwanufaisha watanzania wote.....

Waziri wa maliasili na utalii Angela Kairuki amesema hii ni nafasi kwa serikali ya Tanzania kupitia Mhe Rais  samia kuboresha mazingira rafiki ya uwekezaji na kuendelea kuwavutia wawezekaji na kuongeza idadi ya wawekezaji nchini

Kwa upande wake Mkurugenzi wa bodi ya wakurugenzi ya (TAWA) Hamis Semfuko amesema lazima kuboresha miundombinu ambayo inamilikiwa na tawa ili kuvutia utalii wa ndani katika maeneo mbali mbali…

Mmoja kati ya wawekezaji katika hafla hiyo Taral Abood amesema kupitia uwekezaji huo wanaenda kutekeleza na kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya sita katika kupiga hatua za kimaendeleo…

Hafla hiyo ya utiaji wa saini ya mikataba sita umehudhuriwa na wakala wa misitu tanzania tfs, mamlaka ya usimamizi wa nyamapori tanzania tawa, na wawekezaji pamoja na wadau kutoka sehemu mbali mbali.

Tuesday 2 January 2024

KINANA AWASILI RUANGWA, AHUTUBIA MKUTANO MKUU WA CCM WILAYANI HUMO.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana akiwa ameambatana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Lindi, Hassan Jarifu, wakiwa na viongozi, wanachama wa CCM na wananchi wakienda katika Uwanja wa Likangala mjini Ruangwa kuhudhuria Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Ruangwa. 









MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amewasili wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikakazi ambapo pamoja na mambo mengine atakuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu wa Chama wa wilaya hiyo.

Kinana amewasili wilayani humo leo Januari 1, 2024 akiambatana na viongozi mbalimbali wa Chama wakiwemo baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).

Akiwa wilayani humo kesho atakuwa mgeni rasmi katika Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ya Ruangwa ambao pia utahudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye ni mbunge wa Ruangwa.

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube