BREAKING

Monday 29 October 2018

WATANO WAFARIKI DUNIA KWENYE HELIKOPTA YA MMILIKI WA LEICESTER CITY


Watu  watano wamefariki dunia pamoja na mmiliki wa klabu ya Leicester City ya England, bilionea Vichai Srivaddhanaprabha baada ya helikopta waliyokuwa wamepanda kuteketea kwa moto.

Mmiliki wa Leicester City, Vichai Srivaddhanaprabha, mwenye umri wa miaka 60, ambaye aliinunua klabu hiyo kwa Pauni Milioni 39 mwaka 2010 na kuiwezesha kutwaa taji la ubingwa wa Ligi Kuu ya England mwaka 2016 atakumbukwa kama mtu wa kipekee na muungwana.

Mlimbwende, Nursara Suknamai, Msaidizi wake, Kaveporn Punpare na rubani, Eric Swaffer, ambaye hapo kabla alisafirisha familia ya kifalme, na mpenzi wake na rubani mwenzake wake, Izabela Roza Lechowicz wote wamefariki kwenye ajali hiyo.





















KAGERE, OKWI, KAPOMBE WE ACHA TUU, WAMPAPASA MASAU BWIRE......TAIFA


Baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Ruvu Shooting uliochezwa jana  Uwanja wa Taifa,  umeonekana kuwachanganya viongozi wa Simba kwa furaha, Ofisa  habari wa Simba, Haji Manara amehoji ni nani mwingine anayekuja ili aweze kushushiwa mvua ya mabao.

Manara alisema kuwa kwa mwendo huu wa Simba kuna timu itapigwa mabao mengi zaidi ya hayo matano kutokana na aina ya wachezaji waliopo Simba, mbinu za  Kocha, Patrick Auusems kueleweka.

"Simba ni klabu kubwa lazima uiheshimu, nilikwambia ntakujibu baada ya dk 90, umepapapaswa halafu square unashtka, hii ndio Simba tunang'ata, nani mwingine anakuja ? kwa mwendo huu kuna mtu atapigwa nyingi sana zaidi ya bao 5," alisema.

Simba imefanikiwa kuendeleza rekodi yake ya kufunga mabao mengi kwenye ligi ndani ya mechi moja, kwani kwa mechi zote tano ambazo zilichezwa jana timu nyingi zilishinda kwa idadi ya bao 1 huku Simba ikishinda kwa mabao 5-0..

JAMII YA WABARBAIGI WAPATA HATI MILIKI ZA KIMILA ZINAZOWASAIDIA KUPATA MAKAZI YA KUDUM

Diwani wa kata ya Idodi Onesmo Mtatifikolo ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa utoaji wa hati hizo katika kijiji cha Kitisi ambapo jamii ya wabarbaigi wanaishi maeneo hayo nao walipewa hati miliki za kimira na kuanza kukomesha hama hama ya kabili hilo la wafugaji
Wabarbaigi wanaoishi katika kijiji cha Kitisi kata ya Idodi wilaya ya Iringa wameanza kuondokana na mfumo dume baada ya kukubali wanawake kupatiwa hati miliki za kimila za maeneo ambayo wanamiliki mara baada ya kupata elimu kutoka mradi wa LTA wa feed the future
 JAMII ya Wabarbaigi wanaoishi katika kijiji cha Kitisi kata ya Idodi wilaya ya Iringa wakiwa kwenye picha na viongozi mara baada ya kupatiwa hati miliki za kimila za maeneo ambayo wanamiliki mara baada ya kupata elimu kutoka mradi wa LTA wa feed the future

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

JAMII ya Wabarbaigi wanaoishi katika kijiji cha Kitisi kata ya Idodi wilaya ya Iringa wameanza kuondokana na mfumo dume baada ya kukubali wanawake kupatiwa hati miliki za kimila za maeneo ambayo wanamiliki mara baada ya kupata elimu kutoka mradi wa LTA wa feed the future unaotekelezwa katika wilaya za mkoa wa Iringa na Mbeya.

Wakizungumza wakati wa kukabidhiwa hati za kimira wanawake wa kibarbaigi walisema kuwa awali walikuwa hawaruhusiwi kumiliki mali yoyote ile bali mali zote zilikuwa zinamilikiwa na wanaume.

“Kwenye kabila letu mila zinawapa sana nafasi wanaume kumiliki mali na vitu vingine na kumfanya wanamke kuwa tegemezi jambo ambalo miaka ya nyuma limerudisha maendeleo nyuma ya wanawake” walisema wanawake hao wa Kibarbaigi

Wanawake hao walisema kuwa baada ya kupata elimu ya upimaji wa ardhi na kuifanya ardhi kuwa na hati miliki imesaidia wanaume wa kabila hilo kuanza kuitambua nafasi ya mwanamke na kumuwezesha mwanamke naye kumiliki mali sawa na wanaume wa kabila la wabarbaigi.

Tunaishukuru serikali na mradi wa LTA kwa elimu waliyoitoa kwa wanaume wa kabila la Barbaigi kwa kukubali wanawake wamiliki ardhi kwa kupewa hati miliki za kimira bila elimu hiyo wanawake sisi tungeendelea kuwa wakina mama wa nyumbani tu.

Naye mwenyekiti wa kabila hilo la wafugaji Shabani Ntasham alisema kuwa kupatikana kwa hati miliki za kimira kumekomesha hamahama ya jamii hiyo pamoja na kumuwezesha mwanamke wa jamii hiyo kumiliki ardhi.

“Sisi kabila letu ni watu wa kuhama hama hivyo baada ya kupata hati miliki za kimira sasa hatuwezi kuhama tena kwa kuwa tunamiki ardhi kisheria zinazotuwezesha kuboresha makazi yetu na kutufanya tuishi na kufanya shughuli zetu sehemu moja” alisema Ntasham

Ntasham alisema Mradi wa LTA wa feed the future unaofadhiwa na USD umetoa elimu kwa kabila la barbaigi na kusaidia kuanza kuondokana kwa kiasi chake mfumo dume kwa kuwawezesha wanaume wa kabila hilo kuwagawaia wanawake ardhi na kuzikatia hati miliki za kimila.

“Saizi umeona wanawake na wanaume wanafuraha kwa pamoja kwa kuwa kila mmoja anamiliki ardhi yake ambayo inamuwezesha kufanya jambo analolitaka kwa wakati wake tofauti kama ilivyokuwa hapo zamani” alisema Ntasham

Akizungumza na wanakijiji hao baada ya kukabidhi hati hizo diwani wa kata ya Idodi Onesmo Mtatifikolo alisema kuwa hati hizo zitawasaidia kutenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali kwa kuzingatia uwezo wa ardhi kuhimili idadi hiyo na kasi ya ongezeko la watu na mifugo kwa miaka mingi ijayo.

Mtatifikolo aliongezea kuwa,hatua hiyo itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi kwa kuimarisha usalama wa miliki za ardhi na kuongeza thamani ambayo itawawezesha hata kukopesheka katika taasisi za kifedha zikiwemo benki.

“Usajili wa ardhi ni muhimu kwasababu unaongeza ulinzi wa umiliki wa ardhi, unawezesha uwekezaji, unaongeza thamani ya ardhi na unapunguza migogoro ya ardhi,” alisema Mtatifikolo

Aidha Mtatifikolo aliwaomba Feed The Future wautanue mradi huo angalau ufike umalize kupima vijiji vyote vya kata hiyo  huku akivikumbusha vijiji vyote vya kata hiyo kuendelea kutoa ushirikiano kwenye miradi ambayo inasaidia kukuza maendeleo ya nchi. 

“Tunataka katika kipindi ambacho Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) tuhakikishe tunapima ardhi na mipango ya matumizi bora na ipimwe ili kila mwenye kipande chake cha ardhi awe na hati yake,” alisema Mtatifikolo.

Mtatifikolo aliwataka wanakijiji wa kijiji hicho ambao hawajapimiwa maeneo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubishi na migogoro ya kifamilia kutumia vizuri muda ambao bado mradi huo upo katika wilaya hiyo na kuhakikisha nao wananufaika na zoezi hilo.

Awali naibu mkurugenzi wa Mradi wa LTA, Malaki Msigwa aliwapongeza wataalamu wa mradi huo kwa kuhakikisha wanawasaidia wananchi wa kijiji cha Kitisi kupima maeneo yao na kupata hati miliki za kimila ambazo zitakuwa msaada mkubwa kwenye maendeleo ya kiuchumi.

“Baadhi ya miradi imeibuliwa wakati wa upimaji wa ardhi hivyo ni fursa sasa kwa wananchi wenyewe kuitumia vizuri ardhi waliyopimiwa na kupewa hati miliki za kimila na kwa kuwa asilimia fulani kijiji hiki kimepimwa hivyo wanaweza kuwa kijiji cha mfano kwa kuwapa maendeleo hata wawekezaji wazuri kwa faida yao” alisema Msigwa

Friday 12 October 2018

DKT TIZEBA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI HATI YA MARIDHIANO UKOPESHAJI WA MATREKTA


Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi katika Ukumbi mdogo wa Mikutano Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro leo tarehe 11 Octoba 2018. 


Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa Benki ya Maendeleo ya kilimo (TADB), Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Ndg Marco Mtunga na Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Prof Damian Gabagambi wakionyesha hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi katika Ukumbi mdogo wa Mikutano Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro leo tarehe 11 Octoba 2018.


Naibu Waziri wa kilimo Mhe Omary Mgumba akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi katika Ukumbi mdogo wa Mikutano Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro leo tarehe 11 Octoba 2018.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kushuhudia utiaji saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi katika Ukumbi mdogo wa Mikutano Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro leo tarehe 11 Octoba 2018.

Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba leo tarehe 11 Octoba 2018 ameshuhudia utiaji saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika Ukumbi mdogo wa Mikutano katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro Waziri Tizeba amesisitiza matrekta hayo kutumika ipasavyo kwenye sekta ya kilimo ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa kilimo nchini jambo litakalokuwa na manufaa kwa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Taasisi ambazo zimeshirikiana kufanikisha utiaji saini huo ni Bodi ya Pamba ambayo ipo chini ya wizara ya kilimo, Benki ya Maendeleo ya kilimo-TADB, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Tume ya Maendeleo ya ushirika.

Dkt Tizeba alisema kuwa Vyama vya ushirika vya msingi vinapaswa kuongeza juhudi katika kilimo ili kuakisi kulipa gharama za mkopo ambao ni asilimia 20 ya mkopo wote katika kipindi cha miaka mitatu huku asilimia zingine 80 zikilipwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo-TADB.

Utiaji huo wa saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta 300 kwa vyama vya msingi vya ushirika unajili wakati ambapo hivi karibuni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa alimkabidhi Waziri wa kilimo Dkt Charles Tizeba jumla ya matrekta 500 ya Ursus kwa ajili ya kukopeshwa kwenye  vyama vya ushirika vya msingi ili wakulima kunufaika na tija katika kilimo hususani zao la Pamba.

Akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini Dkt Tizeba alisema kuwa sekta ya kilimo nchini bado inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo tija ndogo inayosababishwa na matumizi madogo ya pembejeo, huduma duni za ugani na matumizi ya zana duni za kilimo ambapo wakulima wengi wanatumia majembe ya mkono au kutumia maksai wakati wa kulima.

“Katika kilimo cha Pamba msimu wa mwaka 2017/2018 ushahidi unaonyesha wakulima walichelewa kuanza kuandaa mashamba kwa sababu Maksai wakati wa kiangazi wanadhoofu sana,” Alikaririwa Dkt Tizeba na kuongeza kuwa

“Mara mvua inaponyesha hawawezi kulima mpaka majani yawe mengi ndio wapate nguvu za kuanza kulima, hali hii inaondoa uwezekano wa wakulima kutumia teknolojia mpya katika kilimo kama vile kilimo hifadhi ambacho kimedhihirika kuongeza tija zaidi ya mara mbili” 

Tizeba alisema mtazamo wa mpango huo ni kuunganisha nguvu za mkulima mmoja mmoja ili kuharakisha kuleta maendeleo yao ambapo utatekelezwa kwa kutumia sehemu ya fedha zinazolipwa AMCOS kama kamisheni ya kusimamia ununuzi wa pamba ambapo matarajio ni kukusanya Bilioni 6 kama uzalishaji wa pamba utafika kilo milioni 400 kwa mwaka.

Alisisitiza kuwa Bodi ya Pamba pamoja na Tume ya Maendeleo ya ushirika zinapaswa kufuatilia kwa karibu hatua zote mwenendo wa ufanyaji kazi wa matrekta hayo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa punde yanapoanza kufanya kazi yawe yanafanyiwa marekebisho ya mara kwa mara.


DSTV WAENDELEA KUWAPA RAHA WATANMZANIA ,MECHI YA STARS NA CAPE VERDE ITAKUWA LIVE SUPERSPORT10

Habari  njema kwa kuwa  Watanzania wataishuhudia timu ya taifa, Taifa Stars Mubasharaa ikiivaa Cape Verde ugenini, kesho.

Mechi hiyo ya kuwania kufuzu Afcon, itaonyeshwa moja kwa moja na chaneli ya SuperSport10 kupitia king'amuzi cha Dstv.

Katika taarifa iliyotolewa na Multichoice Tanzania, mechi hiyo itarushwa moja kwa moja kutoka mjini Praia kuanzia saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Watanzania wengi wapenda michezo na hasa soka walikuwa wakiuliza kama mechi hiyo itarushwa moja kwa moja lakini sasa wana uhakika wa mambo kwamba wataishuhudia mechi hiyo muhimu ya kuwania kufuzu kucheza Afcon, mwakani.

Wednesday 10 October 2018

MAWAZIRI WA SEKTA YA KILIMO WATUAMA JIJINI DODOMA KUJADILI UTEKELEZAJI WA ASDP AWAMU YA PILI



Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu Mhe Jenista Mhagama (Mb)  akizungumza jambo wakati akifungua kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelzaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal-WK)
Kutoka kushoto ni waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mhe Willium Lukuvu (Mb), Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) na Naibu waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji wakifatilia kwa umakini kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelzaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akieleza umuhimu wa kuanza haraka utekelezaji wa ASDP II wakati wa kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelzaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018.
Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mhe Willium Lukuvu (Mb), akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelezaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018. Mwingine ni Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba.
Naibu waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji akieleza utayari wa ushiriki wa wizara yake wakati wa kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelzaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018.
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu Mhe Jenista Mhagama (Mb)  akizungumza jambo wakati akifungua kikao cha Mawaziri wa sekta za kilimo juu ya utekelzaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) leo tarehe 10 Octoba 2018.

Na Mathias Canal, WK-Dodoma

Mawaziri wa wizara za sekta ya kilimo leo tarehe 10 Octoba 2018 wametuama  kwa masaa kadhaa Mjini Dodoma katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kujadili kwa kina kuhusu maandalizi ya utekelezaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II).

Wizara washirika katika kutekeleza ASDP II ni pamoja na Wizara ya kilimo, Wizara ya mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Biashara, na Uwekezaji Wizara ya Maji, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, na Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Utekelezaji wake utachagizwa pia na Wabia wa maendeleo, Sekta binafsi, Taasisi zisizo za kiserikali, Wakulima, Wafugaji na Wavuvi.

Mawaziri hao wakiongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu Mhe Jenista Mhagama (Mb) wameridhia kwa pamoja kuanza haraka utekelezaji wa mradi huo wa ASDP II ambao utakuwa chachu ya ukuzaji wa uchumi kupitia kilimo.

Majadiliano hayo yalijikita zaidi kujadili mapendekezo ya kikao cha makatibu wakuu wa wizara za sekta ya kilimo kilichofanyika tarehe 30 Agosti 2018 pia kujadili namna bora ya Uratibu wa ASDP II, na Mikakati ya kutafuta fedha za kugharamia utekelezaji wa ASDP II.

Katika Mkutano huo Mwenyekiti ambaye ni Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu Mhe Jenista Mhagama (Mb) aliitaka timu ya ASDP II Taifa kueleza kwa kina mikakati ya kuboresha masoko ya mazao ya kipaumbele yaliyoainishwa katika utekelezaji wa ASDP awamu ya pili.

Alisema kuwa kumekuwa na uhamasishaji mkubwa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kulima pindi unapofika msimu wa kilimo lakini bado hamasa ya kutafuta masoko ni ndogo jambo ambalo linageuka karaha kwa wakulima nchi hivyo muarobaini wa kutafuta masoko ndio njia pekee ya kumkomboa mkulima.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akizungumza katika kikao hicho alisema kuwa “ Majira ya Nchi yetu tunaendeshwa na msimu wa kilimo hivyo tunapaswa kutekeleza mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo kwa haraka ili kuendana na msimu” Alisema

Aidha, alisema kuwa punde utekelezaji utakapoanza wafadhili wa mradi huo wanapaswa kupewa uhuru wa kuchagua eneo watakalosaidia ili kuongeza chachu na ufanisi wa haraka katika uwajibikaji.

Naye Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji amewahakikishia mawaziri hao wa sekta za kilimo kuwa, wizara yake imejipanga vyema katika utekelezaji wa Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II).

“ Wengi wamezoea kuiita wizara yetu kama wizara ya madeni sasa tumejipanga vyema katika utekelezaji wa ASDP II kwani tunaamini kabisa kuwa ili kuwa na uchumi mzuri ulioimarika kwa wananchi na Taifa kwa ujumla tunahitaji kuwa na kilimo madhubuti “ Alikaririwa Dkt Kijaji

ASDP II inalenga katika mnyororo wa thamani wa mazao ya kipaumbele na ikolojia ya kanda ya kilimo tofauti na utekelezaji wa ASDP awamu ya kwanza ambao ulifanyika nchi nzima na kuwa na miradi karibu sekta ndogo zote za serikali na vipaumbele na maamuzi ya uwekezaji wa Mamlaka za serikali za mitaa.

Katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa ASDP II Mazao ya kipaumbele yaliyochaguliwa kwa kilimo ni Mchele, Mahindi, Mtama/Uwele, Muhogo, Mboga/Matunda, Mazao ya Mbegu za mafuta (Alizeti, Ufuta, Nazi, Michikichi n.k) Pamba, Kahawa, Sukari, Korosho, Chai, Viazi mviringo na vitamu, Mikunde, Ndizi, na kwa Mifugo na Uvuvi ni Maziwa, Nyama (Ng’ombe), Mbuzi na Kondoo, Kuku, samaki na Mwani.

Malengo ya ASDP II ni kuleta mageuzi ya sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili kuongeza uzalishaji na tija, kufanya kilimo kiwe cha kibiashara zaidi na kuongeza pato la wakulima wadogo kwa ajili ya kuboresha maisha yao, usalama wa chakula na lishe.

Tuesday 9 October 2018

STARS KUPAA KUELEKEA CAPE VERDE USIKU LEO..


Serikali imewaomba  watazania kuendelea kujitokeza Kwenda nchini Cape Verde kuishangilia  timu ya taifa ya Tanzania,Taifa stars 

Akizungumza na wandishi wa habari jinin Dar es salaam Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini Yusuph Singo amesema bado nafasi ipo wazi kwa watanzania kusafiri na timu kesho kuelekea Cape Verde.

Kwa upande wake makamu wa raisi wa TFF amewatoa hofu watanzania kuhusiana na maandalizi ya mchezo huo.

Stars itaondoka kesho saa tano usiku na ndege ya serikali kuelekea nchini Cape Verde na itashuka dimbani kuwakabili wenyeji hao oktoba 12.

KONGAMANO LA AJIRA BINAFSI LAFANYIKA MKOANI MOROGORO

DSC_0006
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe, akifungua kongamano la siku moja la ajira binafsi  mjini Morogoro juzi, lililoandaliwa na Taasisi ya WICOF inayojishughulisha na masuala ya kijamii hususani, walemavu na  watoto  mkoani humo .DSC_0015
Washiriki wa kongamano hilo.
DSC_0018

DSC_0019
Kongamano likiendelea.
DSC_0020

DSC_0022

DSC_0024

DSC_0033
Mtoa mada Mogani Isdori akitoa mada kuhusu ulipaji kodi.
DSC_0055
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akitoa mada kuhusu matumizi ya mitandao.
DSC_0062
Mwanachuo cha Jordan cha mjini Morogoro, Aviva Chrispin akiuliza swali.
DSC_0068
Mjasiriamali, Neema Heri akitoa ushuhuda wa mafanikio yake.
DSC_0070
Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo SUA, Dk.Suleiman Rashid akitoa mada kuhusu umuhimu wa vifungashi kwenye Tangaza na kuongeza thamani ya bidhaa.
DSC_0080
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza katika kongamano hilo akizungumzia umuhimu wa vifungashio na kuongeza thamani ya bidhaa.
DSC_0083
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka  akiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa kongamano hilo, DC Mchembe pamoja na watoa mada.
DSC_0092

Mjasiriamali, Sara Ngonyani akitoa mada.
DSC_0114

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Mwajabu Dhahabu, akihutubia.
DSC_0129
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe, akimkabidhi zawadi ya saa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo.
DSC_0139
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WICOF, Mwajabu Dhahabu akimkabidhi zawadi ya picha baba yake Mzee Dhahabu.
DSC_0144
Picha ya pamoja.
DSC_0149
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo, akiwa katika picha ya pamoja na vijana walioshiriki katika kongamano hilo.
DSC_0156
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo, akiwa na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Gairo.
DSC_0160
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo, akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WICOF.

WANAWAKE nchini wametakiwa kuthubutu, kuwa wavumilivu na wabunifu ili waweze kuinuka kiuchumi.

Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe mjini Morogoro juzi wakati akifungua kongamano la siku moja la ajira binafsi lililoandaliwa na Taasisi ya WICOF inayojishughulisha na masuala ya kijamii hususani, walemavu, watoto na wazee   mkoani Morogoro.

"Ili mjikomboe kiuchumi mnatakiwa kuthubutu, kuwa wavumilivu nawabunifuna uiunga katika vikundi vya ujasiriamali muweze kupata mikopo nakufanyashughuli mbalimbali za biashara" alisema Mchembe.

Alisema dhana ya  50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake si kuosha vyombo bali ni mwanamke kuweza kufanya kazi za uzalishaji mali kama wanavyofanya wanaume na kumiliki ardhi.

Akizungumza wakati akitoa mada katika kongamano hilo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo aliwataka wanawake hao kutumia mitandao ya kijamii kwa maufaa badala ya kuitumia kwa masuala yasiyo na tija.

"Jamani wanawake wenzangu tutumie simu zetu kwa ajili ya maendeleo, kama kupeana taarifa, kutafuta masoko ya bidhaa zetu na si vinginevyo" alisema Mgongo.

Akitoa zawadi ya pekee katika kongamano hilo alisema kwa kutambua umuhimu wa mtoto wa kike Shule ya John The Baptist Girls High School imetangaza fursa ya kusomesha bure wanafunzi  watatu wa kidato cha kwanza na watatu wengine hadi cha nne kwa mwaka 2019.

Alisema anachotakiwa kufanya mwanafunzi ni kufika shuleni hapo siku yoyote ndani ya mwezi wa oktoba 2018 kwa ajili ya kufanya mtihani wa kuchuana na kuwa fursa hiyo imetolewa na Mfuko wa Ndibalema John Mayanja Memorial Scholarship.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Mwajabu Dhahabu alisema kuwa kongamano hilo lenye lengo la kuwajengea uwezo ajira binafsi watoto wa kike ni la kwanza tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo mwaka jana.

Alisema kufanyika kwa kongamano hilo ni maandalizi ya kuelekea katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike duniani yatakayofanyika hivi karibuni.s

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akizungumza katika kongamano hilo alisema serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk.John Magufuli imeweka mazingira mazuri ya kuwasaidia wajasiriamali na kuwa imetenga fedha  kwa ajili ya kuwakopesha hivyo akato mwito kwa wajasiriamali hao kuongeza thamani ya bidhaa zao kwa kuziweka katika vifungashio vilivyobora. 

Katika hatua nyingine Mtaka aliipongeza kampuni ya Trumark kwa kazi kubwa inayoifanya ya kuwasaidia vijana  kuzitambua fursa za maendeleo na akatoa mualiko kwa wajasiriamali hao kwenda Simiyu kwenye maonyesho ya viwanda vidogo vidogo (SIDO) yatakayofanyika kuanzia Oktoba 23 hadi 28.

Kongamano hilo lilihitimishwa kwa makundi mbalimbali pamoja na watoa mada kupata zawadi na vyeti vya ushiriki. 
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube