BREAKING

Tuesday 11 April 2017

YANGA YAITAKA TAKUKURU KUICHUNGUZA KAMATI YA MASAA 72 JUU RUFAA YA SIMBA KWA KAGERA SUGAR


Kamati ya utendaji ya klabu ya soka ya Yanga imesema imepeleka ripoti TAKUKURU ya kuchunguzwa kwa kamati ya masaa 72 ya TFF,Juu ya rufaa ya klabu ya soka ya Simba ambayo imemkatia mchezaji wa kagera Sugar Faki Faki,ambaye Simba wanadai mchezaji huyo alichezeshwa akiwa na kadi za njano tatu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjumbe wa kamati ya utendaji wa Yanga Salum Mkemi amesema kuwa hawana imani na kamati hiyo kwa kuwa inaonyesha kuwa na chembe chembe ya rushwa,ambayo inataka kuipa simba pointi tatu kutoka kwa Kagera,ambao waliifunga Simba mabao 2-1.

Aidha Mkemi ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa iwapo Simba watapewa pointing hizo za mezani watachukua hatua Kali kama klabu.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube