BREAKING

Tuesday 18 April 2017

SAMATTA HUENDA AKAJIUNGA NA FENERBEHCE YA UTURUKI KUCHUKUA NAFASI YA VAN PERSIE,


Fenerbehce ya Uturuki imeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambulizi Mtanzania, Mbwana Samatta anayekipiga KRC Genk ya Ubelgiji ambako amekuwa aking'ara.

Kwa sasa, mkongwe Robon van Persie ndiye kiongozi wa ushambulizi katika timu hiyo ya pili kwa ukubwa nchini Uturuki baada ya Galatasaray.

Lakini  Fenerbehce  inaonekana imeamua kujiimarisha na sasa inasaka mshambulizi kijana na hatari, Samatta anatupiwa jicho.


Wengine ambao wanapewa nafasi ya kusajiliwa na Fenerbehce  ni Thomas Bruns, Theo Bongoda na Ridgeciano Haps.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube