BREAKING

Friday 13 November 2015

MVUA ZAHAIRISHA MECHI KATI BRAZIL NA AGERNTINA




Mchezo wa kuwania kufuzu kwa kombe la dunia kati ya Brazil na Argentina umeahirishwa kufuatia mvua nyingi kunyesha, na kusababisha kujaa kwa maji .

Mchezo huo ulikuwa  usiku wa siku ya alhamisi katika uwanja wa Estadio Antonio Vespucio Libert, mjini Buenos Aires sasa utachezwa usiku wa siku ya ijumaa.

Sehemu ya kuchezea ya uwanja huo ulijaa maji na washabiki wa soka pamoja na maafisa wa timu ya Brazil walikwama njiani kwenye foleni sababu ya mvua kubwa iliyonyesha.

Kocha msaidizi wa Brazil Gilmar Rinaldi, alisema "tulikutana na maafisa wa soka wa Argentina tukazungumza na hakukua na namna ya mchezo kuchezwa.

Katika mchezo huu Argentina itamkosa Nahodha wake Lionel Messi anayesumbuliwa na maumivu wakati Brazil itakuwa nae tena Nahodha wao Neymar Jr ambae hakucheza Mechi 2 za mwanzo akutokana na kuwa adhabu ya kutocheza michezo minne.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube