BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Tuesday, April 08, 2025

Thursday, 12 November 2015

TIKETI ZA STARS, ALGERIA KUUZWA KESHO



Tiketi za mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia chini Urusi mwaka 2018 kati ya Tanzania dhidi ya Algeria ziataanza kuuzwa kesho Ijumaa katika vituo 10 viliyopo jijini Dar es salaam.

Magari maalumu yenye stika yataanza kuuza tiketi hizo za mchezo kesho saa 2 kamili asubuhi mpaka saa 12 jioni, ambapo tiketi zinauzwa kwa shilingi elfu tano (5,000) kwa viti vya rangi ya bluu na kijani na rangi ya machungwa, na elfu kumi (10,000) kwa viti vya VIP B & C.

Vituo vitakavyotumika kuuza tiketi hizo ni ofisi za TFF – Karume, Buguruni – Oilcom, Mbagala – Darlive, Mnazi Mmoja, Luther House – Posta, Big Bone – Msimbazi, Ubungo – Oilcom, Makumbusho – Stand ya Daladala, Uwanja wa Uhuru.

TFF inawaomba wadau, washabiki na watanzania kujitokeza kwa wingi kununua tiketi za mchezo huo katika magari maalumu yatakayokuwepo kwenye vituo vilivyotajwa, ili kuondokana na tatizo la kuuziwa tiketi zisizokuwa halali.

Wakati huo huo Ubalozi wa Algeria nchini Tanzania, umewataka waandishi wa habari wanaotrajia kwenda kuripoti mchezo wa marudiano jijini Algiers siku ya jumanne, kuwasilisha maelezo ya chombo wanachofanyia kazi pamoja na vifaa watakavyovitumia kwenye mchezo huo (camera, vinasa sauti) kuwasilisha maelezo hayo leo Alhamsi kabla ya saa 9 mchana katika ofisi za Ubalozi huo kwa ajili ya kupatiwa Accreditation za kufanyia kazi.

Matokeo ya mchezo wa jana  Azam Sports Federtaion Cup (ASFC), ni Mshikamano 0 - 1 Cosmopolitan,

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube