BREAKING

Saturday 19 December 2020

AZAM FC YA MSEMAJI ZAKA ZA KAZI NA ILE YA LWANDAMINA INAVYOSHANGAZA....

 


Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini alikuwa wakwanza kuchaguliwa kidemokrasia na hatimaye akaja kuwa Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ,alifariki 
Desemba 5,mwaka  2013 akiwa na umri wa miaka 95, alikuwa shujaa kila wakati alizungumza kwa staha , alisema maneno kwa adabu na hekima , mafano aliwahi kusema  "I am not a saint, unless you think of a saint as a sinner who keeps on trying.”  akiwa na maana kuwa " Msinihukumu kwa mafanikio yangu, nihukumuni kwa mara ngapi nilianguka na kuinuka tena"Mwisho wa kunukuu, sina maana ya kuzungumza siasa hapa ninachotaka kukizungumza ni kimoja katika soka husuani Msemaji wa Azam FC Zaka za Kazi Vs Lwandamina.... Zaka ni Msemaji hodari, lakini Lwandamina ni Kocha Mahiri wa Azam FC vitendo vya Lwandamina na Zaka ni Mbingu na Ardhi wakati Zaka akituaminisha msimu huu ubingwa unatua ndani ya klabu hiyo kocha wao Mzambia akili yake wala haimsikilizi kwani hadi sasa Azam FC sare zao ni mfanano wa Maua jana Azam FC ilikubali sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Desemba 18, Uwanja wa Azam Complex, ukiwa ni mwendelezo wa matokeo mabovu kwa Lambalamba hao

Katika mchezo wa jana nyota njema ilianzia kwa Nyota wa Azam FC Ayub  Lyanga alikuwa wa kwanza kucheka na nyavu dakika ya 34, bao hilo lilidumu mpaka muda wa mapumziko na kuwafanya vijana wa Charles Mkwasa kwenda vyumba vya kubadilishia nguo wakiwa nyuma kwa bao moja.

 Kipindi cha pili Iliwachukua dakika 7 Ruvu kuweka mzani sawa kupitia kwa Emmanuel Martin baada ya kipindi kuanza kwa kufunga bao dakika ya 53 ambalo lilidumu kwa muda wa dakika 7 likapinduliwa na Mudahthiri Yahya dakika ya 60.


Ruvu walitumia dakika 10 kusawazisha bao hilo ambapo dakika ya 70 Fully Zully Maganga aliweka mzani sawa na kufanya ubao usome 2-2.

Ni Idd Seleman kwa Azam FC alionyeshwa kadi ya njano huku wajeda wanne walionyeshwa kadi za njano kutokana na nguvu na spidi ndani ya Uwanja wa Azam Complex.


Hii inakuwa ni sare ya pili mfululizo kwa Azam FC ndani ya Uwanja wa Azam Complex baada ya mchezo wao uliopita kufanya hivyo mbele ya Namungo FC na iligawana pointi mojamoja kwa kufungana mabao 2-2.

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ibaki nafasi ya pili ikiwa imecheza mechi 16 kibindoni ina pointi 29 huku Ruvu ikiwa nafasi ya nne na pointi 25 nayo pia imecheza michezo 16.


DORTUMUND YAOKOTWA JALALANI TENA,MOUKOKO AWEKA REKODI YAKE

Mshambuliaji kinda wa Klabu ya Borussia Dortmund, Youssoufa Muokoko  usiku wa kuamkia leo amefunga bao la kwanza ndani ya Ligi ya Uingereza maarufu kama Bundesliga na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo kufunga kwenye ligi hiyo.

Nyota huyo mwenye miaka 16 amevunja rekodi ya nyota wa Bayer Leverkusen, Florian Wirtz ambaye alifunga akiwa na miaka 17 ilikuwa dhidi ya Bayern Munich akiwa  Mei 2020.

Dortmund ambayo ilimchimbisha kocha wao Lucien Favre wiki iliyopita baada ya kupokea kichapo cha mabao 5-1 dhidi ya VfB Stuttgard nafasi iliyochukuliwa na Edin Terzic ilifungwa mabao 2-1 dhidi ya Union Berlin na Moukoko alifunga bao lake la kwanza.

Nyota huyo mzaliwa wa Cameroon amesema kuwa ni furaha kubwa kwake kufunga kwenye mchezo huo ilikuwa dakika ya 60 licha ya timu yake kupoteza jambo ambalo litawafanya wapambane kwa ajili ya mechi zao zijazo.

Mabao ya wapinzani wao yalipachikwa na Taiwo Awonyi dakika ya 57 na lile la ushindi lilipachikwa dakika ya 78 na Marvin Friedrich alipachika bao la ushindi na kuifanya Union Berlin kusepa na pointi tatu mazima Uwanja wa Alle Forsterel.

Matokeo hayo yanaifanya Dortmund iwe nafasi ya nne na pointi 22 baada ya kucheza mechi 13 Bayer Leverkusen  ni vinara wakiwa na pointi 28.



JUMLA YA VIJANA 2000 KUTOKA MKOA WA IRINGA KUFIKIWA NA MRADI WA LYRA IN AFRCA

 

Msimamizi wa mradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue akitoa elimu kwa baadhi ya vijana waliopo kwenye mradi huo
Msimamizi wa maradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue akitoa elimu kwa baadhi ya vijana waliopo kwenye mradi huo
Baadhi ya vijana washiriki wa mafunzo yanayotolewa na
maradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA.

 

 Na Fredy Mgunda,Iringa

JUMLA ya vijana 2000 kutoka kwenye wilaya tatu za mkoa wa Iringa kufikiwa na mradi wa imarika kijana wa LYRA IN AFRCA  wenye lengo la kufungua fikra na mitazamo chanya kwa vijana katika Maisha yao.

 

Akizungumza wakati wa kutoa mafunzo kwa baadhi ya vijana ambao wapo kwenye mradi huo, msimamizi wa mradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuwawezesha vijana kutambua fursa zilizopo na kuzifanyika kazi kwa kupata matokeo chanya.

Alisema kuwa mradi huo unafadhiliwa na watu wa uingereza kwa kuwezesha kutoa mafunzo mbalimbali kwa vijana ambao watakuwa wanatoa elimu kwa vijana na watu wengine kutoka kwenye jamiii ambayo wanaishi huko vijijini kwao.

Mafue alisema kuwa wameshafanikiwa kufanya mafunzo kwa vijana wa vijiji kumi na moja kutoka katika wilaya ya Iringa na Kilolo ambopo hadi sasa takribani vijana 401 wameshafikiwa katika awamu ya kwanza wakitegemea kuanza awamu ya pili mwaka 2021 mwezi wa pili kwa lengo la kufikia vijana wote waliolengwa na mradi.

Alisema kuwa lengo kuu mradi huo ni kuwawezesha vijana kuzitambua fursa zilizopo katika maeneo wanaishi na kuzigeuza kuwa fursa kiuchumi na kukuza maendeleo na kusaidia vijana wasikimbilie mijini na kuzitelekeza fursa zilizopo vijijini.

Mafue alisema kuwa mradi huo unahusisha vijana wenye umri wa miaka kumi na tano hadi ishirini na nane ikiwajumisha vijana walemavu na mzazi mmoja ambao hawana fursa yoyote na kuwasaidia kisaikolojia kuanza kuzichangamkia furs ana kujikombo kimaisha.

“Tunawasaidia pia mzazi mmoja ambaye alipata mimba akiwa shuleni au akiwa na umri mdogo kuzitambua furs ana kuzitumia ili kujikomboa kiuchumi na matumaini kwa vijana wanaoishi vijijini yameongezeka kwa vijana hao kuanza kufanya biashara za kiuchumi” alisema Mafue

 

Alisema kuwa mafunzo ya imarika vijana yamesaidia uundwaji wa vikundi vya kiuchumi ambapo hadi sasa jumla ya vikundi 21 tayari vimeundwa na vinafanya vizuri katika kukopa na kukopesha kwa lengo la kuinua kiuchumi.

Shuhudia Chang’a anatokea Kijiji cha Imalutwa alisema kuwa mafunzo hayo yamekuwa na faida ya kusaidia kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ya kiuchumi tofauti na ilivyokuwa hapo awali kabla ya kupata mafunzo kutoka LYRA IN AFRICA.

Naye Yasinta Migodela alisema kuwa mafunzo hayo yamemsaidia kuboresha ufanisi wa kibiasha kwa kuwa hapo awali alikuwa anafanya biasha bila ya kuwa na mafunzo na kumpelekea kupata hasara lakini baada ya kupata mafunzo yamsaidia jinsi ya utunzaji wa fedha na mpangilio mzima wa biashara.

Kwa upande wao Stanslaus Mtweve,Nestory Simagunga,Cassian Kihongosi na Rebeka Mbwilo walisema kuwa mafunzo waliyopata kutoka katika shirika la LYRA IN AFRICA yamewasidia kuwakomboa kiuchumi na kifikra kutokana na elimu waliyopewa.

 

“Mara baada ya kupewa mafunzo hayo na shirika la LYRA IN AFRCA yalitusaidia kuridi katika vijiji vyetu na kuendelea kutoa elimu kwa jamii yetu ambao kwa asilimia furani tumesaidia vijana wengi kuacha tabia ya ulevi na matumizi ya madawa ya kulevya na wameanza kujikita katika shughuli za kiuchumi ambazo kwa sasa zinachochea uchumi kukua” walisema

 

 

 

MADIWANI HALMASHAURI MJI MAFINGA WAAHIDI NEEMA YA MAENDELEO KWA WANANCHI WAO

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Mafinga Reginant Kivinge akiongea madiwani,watendaji na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa baraza hilo.

Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini na mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rose Tweve wakiwa kwenye uzinduzi wa baraza hilo la madiwani



MADIWANI wa Halmashauri ya mji wa Mafinga mkoani Iringa wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ili kureta maendeleo kwa wananchi waliwachagua na kuwapa dhamana ya kuwepo madarakani mara baada ya uchaguzi mkuu

Akizungumza mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza jipya la madiwani wa Halmashauri ya mji wa Mafinga,mwenyekiti wa halmashauri hiyo Reginant Kivinge alisema kuwa wananchi wanamatumaini makubwa ya kimaendeleo kutoka kwa madiwani hao hivyo wanapaswa kwenda kuchapa kazi kwa nguvu zao zote.

Kivinge alimuomba mkurugenzi wa halmashauri hiyo Saada Mwaruka  pamoja na watendaji wote kuhakikisha wanashirikiana kwa ukaribu ili kuhakikisha wanatatua na kumaliza kero zote zinazowakabili wananchi.

 

Alisema kuwa halmashauri hiyo bado inakabiriwa na changamoto nyingi ambazo zimekuwa zikikwamisha juhudi za kureta maendeleo kwa wananchi wa jimbo la Mafinga Mjini hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa umoja wao ili kuleta maendeleo kwa wananchi yanayotarajiwa.

  "Natambua uchaguzi huu ulioisha tulipitia mambo mengi sana,lakini sasa uchaguzi umekwisha  ni mwendo wa kuchapa kazi sasa twende kuchapa kazi ili turudishe ile heshima muliyopewa na wananchi wetu kwa kutuchagua " alisema

 

 

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa (CCM) wilaya ya Mufindi mkoa wa Iringa Daudi Yasini amewataka madiwani wa halimashauri ya Mji Mafinga kwenda kushungulika na kutatua kero za wananchi kwani chama hicho hakitasita kumchukulia hatua diwani yoyote asiyetimiza majukumu yake ipasavyo .

Kauli hiyo imetolewa wakati wa kikao cha kwanza cha madiwani wa halmashauri hiyo baada ya kula kiapo cha utii wa kuwatumikia wananchi kwa kufuata kanuni za maadili ya utumishi wa umma

Daudi alisema kuwa wananchi wamekuwa na imani kubwa na chama cha mapinduzi hivyo hivyo wanapaswa kuheshimu na kuthamini nafasi waliyopewa kwa kufanya kazi kwa weredi na ushirikiano kuhakikisha wanatatua kero za wananchi wa halamshauri hiyo.

"Tumekuwa na uchaguzi nyingi ila uchaguzi wa mwaka huu tumeweka historia kwa wilaya ya Mufindi kwa baraza letu lote ni CCM na hii ni kwa sababu ya kazi kubwa iliyofanywa na mh Rais Magufuli hivyo naamini hamtatuangusha mkatumikie nafasi muliyopewa kwa weredi uliotukuka" 

 

Daudi alitoa onyo kali kwa madiwani wote wanaodhani wamepewa nafasi hiyo kwa ajili ya kujinufaisha wao au kujipatia mali katika Halmashauri hiyo,chama cha mapinduzi kitapita kata kwa kata kuhakikisha kuwa viongozi waliochaguliwa wanatatua kero za wananchi la sivyo hatua kali zitachukuliwa kwa Diwani husika.

“Niwaonye wale wote ambao mnadhani mmepata nafasi ya kwenda kupiga dili halimashauri hapa ni kazi tu na endapo tutakuja kwenye kata yako na kukuta wananchi wanalalamika kero nyingi hazitatatuliwa basi hawatasita kuwachukulia hatua” alisema Daudi

Hata hivyo Daudi alimtaka mkurugenzi pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kushirikiana vyema na madiwani hao ili kutatua kero za wananchi zinazowakabili na sio kupishana kwenye maamuzi ya vikao ambavyo lengo ni kupunguza mzigo wa kero kwa wananchi

Naye katibu wa CCM wilaya ya Mufindi James Mgego aliwashukuru madiwani hao kwa uvumilivu na ushindi waliopata kwenye uchaguzi uliopita kwani walipita kwenye viunzi na vikwanzo Vingi mpaka kufika hapo walipo

Mgego alisema kuwa wananchi wamemaliza kazi yao na wajibu wao hivyo sasa ni wakati wa madiwani hao kurudisha dhamana na heshima waliyopewa kwa kwenda kuwatumikia na kutatua kero za wananchi

Alisema chama hicho kinatambua dhamana kubwa waliyopewa na wananchi hao kwa kuonyesha imani kwa chama hicho hivyo wanadeni kubwa la kurudisha maendeleo ya kweli kwa watanzania wote bila kujali itikadi ya vyama kwani uchaguzi umekwisha na sasa ni muda wa kuchapa kazi

Lakini pia Mbunge wa jimbo la Mafinga Cosato Chumi alissema kuwa anataka kupeleka mapendekezo bungeni ili kuweza kupata kibali na kubadili sheria ili kufanya biashara kwa mji wa Mafinga masaa 24 kwani wilaya hiyo inapitiwa na barabara kuu hivyo itakuwa ni fursa ya kukuza uchumi kwa wakazi wa Mafinga na kuongeza pato la halimashauri hiyo endapo watu watafanya biashara masaa 24 

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Mafinga Saada Mwaruka alisema kuwa watendaji wote wa halmashauri hiyo wapo tayari kujitolea na kuonyesha ushirikiano kwa madiwani wote ili kuhakikisha wanatatua kero za wananchi na kuleta maendeleo katika Jimbo la Mafinga Mjini.

 

 

Wednesday 17 June 2020

BABA WA SAMATTA ANENA JAMBO....WAKATI SAMATTA AKIWA UWANJANI LEO EPL

MSHAMBULIAJI wa timu ya Aston Villa inayoshiriki Premier League, Mtanzania, Mbwana Samatta amemhakikishia baba yake mzazi, mzee Ally Samatta kuwa atapambana kuhakikisha anainusuru timu yake isishuke daraja msimu huu.

Samatta ambaye amejiunga na timu hiyo katika usajili wa dirisha dogo msimu huu kwa mkataba wa miaka minne na nusu, ana kazi kubwa ya kuibakisha timu hiyo kutokana na kuwa kwenye nafasi mbaya ya 19 ikiwa na pointi 25 ikifuatiwa na Norwich City ambayo inaburuza mkia ikiwa na pointi 21.

Mzee Samatta alisema kuwa, kutokana na ligi kutarajiwa kurejea tena leo Juni 17, 2020, mtoto wake amemwambia atapambana kuinusuru timu hiyo kushuka daraja.

“Suala la ligi kurejea lipo wazi na kila mmoja amekuwa akilijua vizuri isipokuwa kijana amenieleza nia yake ni kutaka kuinusuru timu isishuke hivyo amepanga kucheza kwa kujituma zaidi ili kufikia malengo.

“Unajua wapo ambao walitaka ligi ifutwe kama zilizofanya nchi nyingine lakini England wao wameona ni bora kumalizia hivyo kila mmoja anatakiwa apambane na yeye ndiye amenieleza kwamba hatamani kuona wakishuka hivyo lazima ajitoe ili kuinusuru timu na msimu ujao waanze pamoja,” alisema mzee Samatta.

WADAU WATAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO







WADAU WAMETAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO  KUWEKA UDHAMINI KWENYE TIMU ZA MTAANI ILI KUIBUA VIPAJI AMBAVYO VITAKUA NA MANUFAA KWA TAIFA 
Kuali hiyo imetolewa katika Mchezo wa Kusisimua uliozikutanisha  timu mbili kati ya Soccer City ya Mabwepande ya Mtaa wa Mji Mpya  dhidi ya timu ya New Kibamba FC Mchezo ambao umedhaminiwa na kampuni ya Msukuma One inayodhalisha na kusambaza Nafaka huku lengo ikiwa kuunga Mkono Serikali ya awamu ya tank kuunga mkono juhudi za kuinua sekta ya Michezo.

Mkurugenzi Mkuu wa Msukuma One Aman Manengero amesema kuwa wataendelea kusaidia jitihada hizo ili kuleta meandeleo zaidi.
Ktika mchezo huo mkali ilishuhudiwa timu ya kibamba FC kukubali kipigo baada ya kuzidiwa kwa mikwaju ya penati dhidi ya timu ya soka city baada ya timu hizo kutoka sare ya 

goli mbili kwa mbili ndani ya dakika tisini huku timu ya soka city ikiibuka na zawadi ya jezi iliyotolewa na mdau huyo.






Tuesday 2 June 2020

NDEGE YA MIZIGO KUIMARISHA USAFIRISHAJI SAMAKI NJE NCHI HIYOOO KUTUA


 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mipango ya Serikali kununua ndege ya mizigo utaimarisha usafirishaji wa minofu ya samaki moja kwa moja kwenda nje ya nchi kutokea uwanja wa ndege wa Mwanza.

Waziri Kamwelwe ameyasema hayo Jumatatu Juni Mosi 2020 jijini Mwanza wakati akifungua mkutano wa kupokea mikakati ya pamoja kuondoa vikwazo na kufanikisha biashara ya usafirishaji minofu ya samaki kwenda nje ya nchi hususani mataifa ya Ulaya ambako kumekuwa na soko la uhakika.

Kikao hicho kimewajumuisha pia Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara za Mifugo na Uvuvi, Viwanda na Biashara pamoja na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (katika) akizungumza kwenye kikao hicho. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na kulia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.


Friday 22 May 2020

LAMPARD HANA NENO NA KANTE,KUJITENGA KUTAZAMA AFYA YAKE






Kocha Mkuu wa Chelsea, Frank Lampard amesema kuwa uamuzi wa kiungo wake N'Golo Kante kujitenga na wenzake ni mzuri kwa manufaa yake na afya za wengine pia.

Kante aliripoti mazoezini siku ya Jumanne katika kituo cha Cobham HQ ila alishindwa kurejea siku ya Jumatano kutokana na kutojihisi vizuri.

Kwa sasa timu nyingi zinazoshiriki Ligi Kuu England zimeanza maandalizi ya kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya kumalizia mechi zilizobaki baada ya ligi kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona .

Habari zinaeleza kuwa sababu kubwa ya Kante kushindwa kuendelea kuripoti mazoezini ni hofu ya kupata maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo bado vinasambaa kwa kasi.

RAIS MAGUFULI ARUHUSU MICHEZO NA VYUO JUNI MOSI....


Rais wa Tanzania, John Magufuli ametangaza kuwa vyuo vikuu nchini humo vitafungufuliwa Juni Mosi, na kuruhusu pia shughuli zote za michezo nazo ziendelee kama kawaida.
Rais Magufuli amesema vyuo vikuu vyote sasa vitarejea katika hali yake ya kawaida kuendelea na masomo kuanzia Juni Mosi baada ya kijiridhisha kutokana na maendeleo ya hali ya maambukizi ya virusi vya corona.
Amesema maambukizi nchini humu yameshuka kwa kiwango cha kuridhisha hatua ambayo imemfanya aanze kufungua baadhi ya shughuli zilizokuwa zimesimama kutokana na janga hilo la virusi vya corona lilipopiga hodi kwa mara ya kwanza nchini Machi 16.
"Ikiwa mwelekeo nnaouona utandelea katika wiki zijazo, napanga kufungua vyuo vikuu ili wanfunzi waendelee na masomo yao, alisema Magufuli wakati akizungumza kwenye ibada ya misa kaskazini-magharibi mwa nchi wiki iliyopita.
Hatua nyingine ambazo Rais Magufuli amezitangata wakati alipokuwa akiwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni ni kuwaruhusu wanafunzi wa kidato cha sita wanaojiandaa na mitihani ya kuhitimu masomo yao kurejea shuleni.

Tuesday 10 March 2020

BRAND KENYA YATUA JIJINI DAR ES SALAAM .....



The High Commissioner of the Republic of Kenya in the United Republic of Tanzania Amb. Dan Kazungu on Monday received a high- level trade mission from Kenya’s Export and Branding Agency, Brand.KE. The trade delegation was led by the Chief Executive Officer Mr. Peter Biwott. The trade mission is in Dar es salaam to hold consultations with key Tanzanian trade and investment promotion organisations in a bid to promote and enhance bilateral trade between Kenya and Tanzania. These include Tanzania Trade and Development Authority (TANTRADE), Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF).
Kenya’s High Commissioner Amb. Dan Kazungu with Mr. Peter Biwott, CEO of Brand.KE holding discussions during the latter’s visit at the Kenya High Commission on Monday9th March 2020
While welcoming the delegation, Amb. Dan Kazungu mentioned that 48 percent of intra East African Community (EAC) trade occurs between Kenya and Tanzania which is an indication of the interdependence that exists between the two countries. He added that there is need for both Kenyans and Tanzanians to cooperate even more for shared prosperity.
On his part, Mr. Biwott said that it was a high time that Kenyans and Tanzanians focused more on cross border trade that would boost each other’s economies more as opposed to seeking foreign markets whose returns were much lower. Mr. Biwott also noted that Kenya and Tanzania are unique countries with vast opportunities ranging from agriculture, infrastructure, services, mining, logistics and the blue economy. In addition, there are opportunities for Kenyan companies in the financial service sector. These opportunities can be seized through partnerships with Tanzanian companies.
Brand.KE is a State Corporation established under the State Corporations Act Cap 446 through Legal Notice No.110 of August 9th, 2019 after the merger of the Export Promotion Council and Brand Kenya Board. The Brand.KE mandate is to implement export promotion and nation branding initiatives and policies to promote Kenya’s export of goods and services.
Brand.KE CEO Mr. Peter Biwott signing the visitor’s book at the Kenya High Commission. With him is Kenya’s High Commissioner Amb. Dan Kazungu
Kenyan companies, through Brand.KE, will participate in the 44th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) slated for June and July 2020. Brand.KE has reserved a substantive number of booths for this years’ event that promises Kenyan high-level participation and a showcase of how trade and investment is undertaken in the East African region and beyond.
The DITF presents Kenyan companies to invest in Tanzania as well as export their goods and services while at the same time, offering opportunities to the Tanzanian private sector in so far as market and product diversification is concerned. Thus, participation in the Trade Fair will enhance trade, investment and tourism with a view to promote accelerated economic growth and development between the two countries and East Africa as well as the African continent.
Brand.KE in conjunction with the Kenya High Commission Dar es Salaam will organize a high-level business forum, an elaborate diaspora engagement and high-level participation at the Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) between March and July 2020. The trade mission will focus its activities in four regions in its bid to boost the distribution channel of Kenyan goods in Tanzania. These include: - Mwanza (Mwanza region), Arusha and Moshi (Kilimanjaro region), Dar es Salaam (Dar es Salaam and Coast regions) and Mbeya (Southern region).
Brand.KE are also planning a second visit that will focus on developing an elaborate distribution channel for Kenyan goods in Dodoma (Central Tanzania) and Zanzibar in a carefully conceived and deliberate strategy to promote Kenyan exports in the United Republic of Tanzania.
Amb. Dan Kazungu receives a gift from Mr. Peter Biwott, CEO of Brand.KE at the Kenya High Commission on Monday 9th March 2020
The Kenya High Commission in Dar es Salaam is upbeat that these efforts will improve the trade performance that stands at Kshs 33.5 billion in January 2020, up from Kshs 28 billion in 2018.

ISUPILO HAKUNA ARDHI YA KUGAWAKWA WANANCHI,MIPAKA YA GEREZA ILINDWE.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ikongosi wilaya ya Mufindi

NA FREDY MGUNDA,MUFINDI.
 
MKUU wa magereza la Isupilo Benjamin Kabisa wamejipanga kulinda ardhi ya magereza kwa kuwa  Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli amegiza kuwa magereza yote kuanza kujitegemea kwa kuzalisha chakula kupitia wafungwa.


Hoja hiyo imekuja mara baada ya wananchi wa kijiji cha Ikongosi wilaya ya Mufindi la kuomba ardhi ya kulima katika eneo la jeshi la magereza kwenye mkutano wa mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi wakati wa ziara ya Iringa mpya awamu ya pili.


Benjamin alisema kuwa eneo la gereza la Isupilo mipaka yake inajulikana na ipo kisheria nay eye hawezi kugawa eneo hilo hadi pale mamla za juu za serikali zitakavyo amua kwa kuwa kila kitu kipo kimaandishi.


Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi alikataa ombi hilo kwa wananchi wa kijiji cha Ikongosi  wakati wa mkutano wa kupokea kero za wananchi wa wilaya ya Mufindi.


Alisema kuwa ardhi ya magereza ni kwa ajili ya matumizi ya magereza kuzalisha chakula kwa ajili ya wafungwa.

hata hivyo Hapi alisema kuwa sio kila ombi la wananchi anatakiwa kuwatekelezea kwani kimsingi ardhi ya magereza ni maalum kwa ajili ya utaratibu wa serikali kuhifadhi ardhi yake kwa ajili ya matumizi yake ya baadae.

"Serikali ina kawaida ya kuwekeza benki ya Ardhi kwa ajili ya matumizi ya kijamii ikija kutokea wananchi wameongezeka na serikali inahitaji kujenga kituo cha afya ama shule benki yake ya ardhi ni kwenye ardhi hiyo iliyowekezwa kwenye taasisi zake kama magereza,jeshi la kujenga Taifa na maeneo mengine"

Aidha alisema iwapo wananchi wanahitaji eneo kwa ajili ya ujenzi wa shule wanaweza kukaa chini na Magereza ili kupewa eneo Ila sio kwa ajili ya kilimo .

Alisema kimsingi shule ni mali ya serikali na magereza ipo chini ya serikali hivyo wanaweza kupewa eneo la ujenzi na kuwekewa mipaka.

"Ila niwaeleze wazi wananchi kuwa sio kila ombi mnaloomba mnaweza kusikilizwa maombi mengine hayawezekani kama hili la kuomba ardhi ya magereza kwa ajili ya kulima  watu binafsi"


Hata hivyo Hapi aliagiza magereza kutumia wafungwa kuendeleza ardhi hiyo kwa kilimo Kama Rais Dkt John Magufuli alivyoagiza kwa magereza zote nchini kutumia wafungwa kuzalisha chakula Chao wenyewe.

TARURA SITISHENI UJENZI WA BARABARA ZA VUMBI HADI MVUA ZITAKAPO SIMAMA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akizungumza kwenye ziara ya Iringa mpya awamu ya pili alipokuwa anakagua ujenzi wa barabara yaKinyanambo, Pareto,Chumi,Lutherani na Mwamkoa Mbagala iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga akiwataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara hizo kwa kuwa ujenzi huo hauna tija kwa wananchi
 Baadhi ya uharibifu unaondelea kwenye maeneo ambayo ujenzi wa barabara unaendelea hivi sasa kwenye maeneo ya Mji wa Mafinaga Mji.
 Baadhi ya uharibifu unaondelea kwenye maeneo ambayo ujenzi wa barabara unaendelea hivi sasa kwenye maeneo ya Mji wa Mafinaga Mji

NA FREDY MGUNDA,MUFINDI.

SERIKALI ya mkoa wa Iringa imewataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara za vumbi zinazoendelea kujengwa na wakandarasi mbalimbali kutokana mvua kubwa zinazoendelea hivi sasa.

Akizungumza kwenye ziara ya Iringa mpya awamu ya pili alipokuwa anakagua ujenzi wa barabara yaKinyanambo, Pareto,Chumi,Lutherani na Mwamkoa Mbagala iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga,mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi aliwataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara hizo kwa kuwa ujenzi huo hauna tija kwa wananchi.

Kipindi hiki mvua zinanyesha kwa wingi kila kona na zimekuwa zikiharibu miundombinu katika maeneo mengi katika mkoa huu wa Iringa,hivyo kutokana na hali hiyo natangaza kusitisha ujenzi wa barabara hizo hadi pale mvua zitakapo isha.

Hapi aliwataka viongozi wa TARURA kuhakikisha wanawasimamia vilivyo wakandarasi wote wanajenga barabara hizo ili zijengwe katika ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha iliyotolewa na serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

“Hakikisheni mnawasimamia vilivyo wakandarasi hao kwa kuwa fedha zinazotumika ni kodi za wananchi hao ambao mnawaona hapa,hivyo lazima thamani ya fedha hizo ionekane kwa wananchi hawa” alisema Hapi

Hapi aliwataka TARURA kuongeza kasi ya ujenzi wa mitandao ya barabara za lami katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga na ujenzi wa taa za barabarani ili Halmashauri ya Mji wa Mafinga kuwa Manispaa na hatimaye mkoa wa Iringa kuwa Jiji.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliamu aliwataka TARURA  kujenga mitaro yenye ubora unaotakiwa ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa inamudu maji yote yanayopita na kuzilinda barabara zisiaharibike haraka na zidumu kwa muda mrefu.

“Barabara zetu nyingi za wilaya hii zinaharibika kutokana na kutokuwa na mitaro iliyobora inayohimili maji mengi na ndio maana barabara zinaharibika kila uchwao hizi ni bora kuweni wakali kwa wakandarasi wanaopewa tenda za mitaro kwenye barabara husika” alisema Wiliam

Akijibia hoja za mkuu wa mkoa,mwananchi Inocent Mahanga na mkuu wa wilaya ya Mufindi,meneja wa TARURA Mafinga Tc Injinia Simoni Ngagani alisema kuwa watahakikisha barabara zinajengwa kwenye ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha za mradi husika.

Tutahakikisha ujenzi wa Mifereji na barabara zinajengwa kwa viwango stahili ili kutumia vilizuri kodi za wananchi


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube