BREAKING

Friday 22 May 2020

RAIS MAGUFULI ARUHUSU MICHEZO NA VYUO JUNI MOSI....


Rais wa Tanzania, John Magufuli ametangaza kuwa vyuo vikuu nchini humo vitafungufuliwa Juni Mosi, na kuruhusu pia shughuli zote za michezo nazo ziendelee kama kawaida.
Rais Magufuli amesema vyuo vikuu vyote sasa vitarejea katika hali yake ya kawaida kuendelea na masomo kuanzia Juni Mosi baada ya kijiridhisha kutokana na maendeleo ya hali ya maambukizi ya virusi vya corona.
Amesema maambukizi nchini humu yameshuka kwa kiwango cha kuridhisha hatua ambayo imemfanya aanze kufungua baadhi ya shughuli zilizokuwa zimesimama kutokana na janga hilo la virusi vya corona lilipopiga hodi kwa mara ya kwanza nchini Machi 16.
"Ikiwa mwelekeo nnaouona utandelea katika wiki zijazo, napanga kufungua vyuo vikuu ili wanfunzi waendelee na masomo yao, alisema Magufuli wakati akizungumza kwenye ibada ya misa kaskazini-magharibi mwa nchi wiki iliyopita.
Hatua nyingine ambazo Rais Magufuli amezitangata wakati alipokuwa akiwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni ni kuwaruhusu wanafunzi wa kidato cha sita wanaojiandaa na mitihani ya kuhitimu masomo yao kurejea shuleni.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube