BREAKING

Friday 22 May 2020

LAMPARD HANA NENO NA KANTE,KUJITENGA KUTAZAMA AFYA YAKE






Kocha Mkuu wa Chelsea, Frank Lampard amesema kuwa uamuzi wa kiungo wake N'Golo Kante kujitenga na wenzake ni mzuri kwa manufaa yake na afya za wengine pia.

Kante aliripoti mazoezini siku ya Jumanne katika kituo cha Cobham HQ ila alishindwa kurejea siku ya Jumatano kutokana na kutojihisi vizuri.

Kwa sasa timu nyingi zinazoshiriki Ligi Kuu England zimeanza maandalizi ya kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya kumalizia mechi zilizobaki baada ya ligi kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona .

Habari zinaeleza kuwa sababu kubwa ya Kante kushindwa kuendelea kuripoti mazoezini ni hofu ya kupata maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo bado vinasambaa kwa kasi.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube